Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 7 Youth, Disabled, Labor and Employment Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu 107 2024-02-13

Name

Latifa Khamis Juwakali

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. LATIFA KHAMIS JUWAKALI aliuliza:-

Je, Serikali imefanya tathmini ya mafunzo wanayopatiwa vijana chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu baada ya kumaliza mafunzo?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu naomba kujibu swali la Mheshimiwa Latifa Khamis Juwakali, lililoulizwa kwa niaba yake na Mheshimiwa Rashid Shangazi kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Ofisi ya Waziri Mkuu inatekeleza Programu ya Taifa ya Kukuza Ujuzi nchini ambayo iliandaliwa baada ya kufanya utafiti wa nguvu kazi wa mwaka 2014 ambapo ulionesha kiwango cha ujuzi wa nguvu kazi ya Taifa ni asilimia 3.6 kwa ujuzi wa juu, asilimia 16.4 kwa ujuzi wa kati na asilimia 79.9 ujuzi wa kiwango cha chini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2021/2022 Serikali ilifanya tena utafiti wa nguvukazi na kuonesha kiwango cha ujuzi wa nguvukazi kimeanza kuwa bora na nguvukazi yenye kiwango cha chini cha ujuzi ilifikia asilimia 76.9 ya nguvu kazi kutoka asilimia 79.9 na kiwango cha kati kimefikia asilimia 19.9 ya nguvukazi kutoka asilimia 16.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kujiridhisha na ubora wa mafunzo yanayotolewa kupitia Programu ya Taifa ya Kukuza Ujuzi, Serikali imepanga kufanya tathmini ya mafunzo yanayotelewa kwa kufanya tracer study katika mwaka wa fedha 2024/2025, ahsante.