Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 11 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 189 2024-02-13

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU aliuliza: -

Je, Serikali inatoa kauli gani juu ya malipo ya fidia kwenye miradi ya barabara za TANROADS zinazopita kwenye makazi ya watu Kibamba?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Issa Jumanne Mtemvu, Mbunge wa Kibamba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ulipaji wa fidia kwa wananchi ambao mali zao zinaathiriwa na miradi ya ujenzi wa barabara hufanyika kwa mujibu wa Sheria ya Barabara Namba 13 ya mwaka 2007. Wananchi wote ambao mali zao ziko nje ya eneo la hifadhi ya barabara wanalipwa fidia na wale ambao mali zao zimo ndani ya eneo la hifadhi ya barabara hawastahili kulipwa fidia. Hii ni kwa wananchi wote nchi nzima ikiwemo na wananchi wa Jimbo la Kibamba, ahsante.