Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 11 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 186 2024-02-13

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha inaenzi Tamaduni za Makabila ili kulinda maadili?

Name

Hamis Mohamed Mwinjuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jackson Gedion Kiswaga, Mbunge wa Kalenga, kama ifutavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuhakikisha tunaenzi tamaduni za makabila kwa lengo la kulinda maadili ya Mtanzania Serikali inafanya yafuatayo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwamza ni kuendesha Tamasha la Kitaifa la Utamaduni ambalo hufanyika kila mwaka. Tamsha hilo linashirikisha vikundi vya utamaduni kutoka Mikoa yote ya Tanzania bara na Visiwani, ambalo linahusisha shughuli mbalimbali za kiutamaduni, kama vile maonesho ya vyakula vya asili, urembo na utanashati, michezo ya jadi, teknolojia na sayansi jadia. Pia, Tamasha hilo linahusisha mashindano ya ngoma za asili, upishi na uandaaji wa vyakula vya asili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sambamba na hayo, Tamasha hilo huambatana na mdahalo wa namna ya kupambana na mmomonyoko wa maadili. Hivyo kupitia tamasha hilo, wananchi wanasherehekea, wanaenzi, wanatunza na kuendeleza tamaduni zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mbili Serikali inaendelea kutumia majukwaa mbalimbali kama vile makongamano, semina, mikutano na warsha kutoa elimu kwa jamii kuhusu umuhimu wa kuthamini utamaduni na maadili ya Mtanzania

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu, inaendelea kufanya Tafiti mbalimbali ili kubaini mila na desturi zinazo kubalika katika jamii ili ziendelezwe na zisizofaa waachane nazo, ambapo hadi sasa jumla ya tafiti 286 kuhusu mila na desturi za maeneo ya Kihistoria zimefanyika;

Mheshimiwa Mwenyekiti na mwisho inaendelea kushirikiana na wadau na kuwahimiza kufanya matamasha mbalimbali ya utamaduni nchini kote, ili kuhakikisha mila, desturi na tamaduni zetu zinalindwa na kuendelezwa.