Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 11 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 182 2024-02-13

Name

Charles Muguta Kajege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. CHARLES M. KAJEGE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga Malambo ya kunyweshea mifugo katika Jimbo la Mwibara?

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Charles Muguta Kajege, Mbunge wa Mwibara, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua changamoto ya upatikanaji wa maji ya mifugo katika maeneo mbalimbali hapa nchini ikiwa ni katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda; na aidha katika mwaka 2022/2023 Serikali ilianza ujenzi wa bwawa la maji ya mifugo katika Kijiji cha Kihumbo Halmashauri ya Wilaya ya Bunda ambapo ujenzi wa bwawa hilo umefikia asilimia 95. Kazi inayoendelea kwa sasa ni ujenzi wa mabirika ya kunyeshea maji ya mifugo kabla ya bwawa kuanza kutumika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na jitihada zinazofanywa na Serikali za kujenga mabwawa na kuchimba visima virefu kwa ajili ya maji ya mifugo bado mahitaji ni makubwa. Hivyo nitoe wito kwa Wakurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya kuhamasisha wafugaji na wadau wengine kuwekeza kwenye miundombinu ya maji kwa ajili ya mifugo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.