Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 11 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 172 2024-02-13

Name

Dr. Alfred James Kimea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI K.n.y. MHE. DKT. ALFRED J. KIMEA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Kibo – Mgombezi – Bagamoyo na NMB Benki hadi Magunga hospitali zilizo kwenye mradi wa TACTIC?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Alfred James Kimea, Mbunge wa Jimbo la Korogwe Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara za Kibo - Mgombezi - Bagamoyo na NMB Benki hadi Hospitali ya Magunga zipo kwenye utekelezaji wa mradi wa TACTIC kundi la pili (Tier 2). Kundi hili linatekelezwa kwenye Miji 15 ikiwemo Halmashauri ya Mji wa Korogwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa kazi ya usanifu wa miradi ya ujenzi wa barabara kupitia kundi la pili (Tier 2) unaendelea kutekelezwa na Wahandisi Washauri ambapo tayari walisaini mikataba tarehe 15 Disemba, 2023 na itafanyika kwa kipindi cha miezi nane ambapo kitakamilika mwezi Agosti, 2024. Aidha, usanifu wa miradi hiyo utakapokamilika Agosti, 2024 kazi ya kutangaza zabuni itaanza Septemba, 2024.