Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 7 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 119 2024-03-07

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza: -

Je, Serikali ipo tayari kufanya utafiti wa madini katika Kata ya KIA Jimbo la Hai?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

WAZIRI WA MADINI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Saashisha Elinikyo Mafuwe, Mbunge wa Jimbo la Hai, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) ipo tayari kufanya utafiti wa Jiosayansi katika Wilaya ya Hai. Aidha, GST iko tayari kutoa ushirikiano kwa wadau wa sekta binafsi wenye nia ya kufanya tafiti za madini, kwa kuwapa taarifa za awali kwa kuwa taasisi hii, imefanya utafiti wa awali na kubaini kuwa hadi sasa jiolojia ya Wilaya hiyo inafaa kwa upatikanaji wa mawe ya ujenzi hasa chokaa mfano katika Kata ya Masama Rundugai.