Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 7 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 115 2024-02-07

Name

Tabasamu Hamisi Hussein Mwagao

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sengerema

Primary Question

MHE. TABASAM H. MWAGAO K.n.y. MHE. SHANIF M. JAMAL aliuliza: -

Je, lini Serikali itaanza mchakato wa kutangaza Barabara ya Mabuki – Jojiro hadi Ngudu ili ijengwe kwa kiwango cha lami?

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

WAZIRI WA UJENZI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Shanif Mansoor Jamal, Mbunge wa Kwimba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeanza utekelezaji wa Mradi wa Ujenzi wa Barabara ya Mabuki – Jojiro – Ngudu yenye urefu wa kilomita 28 kwa kiwango cha lami kwa awamu; ambapo mkataba wa ujenzi wa kilomita tatu kuanzia eneo la Ngudu mjini kuelekea Jojiro umesainiwa tarehe 19 Januari, mwaka huu wa 2024. Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuendelea na ujenzi kwa kiwango cha lami kwa awamu kwa sehemu iliyobaki, ahsante sana.