Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 7 Information, Communication and Information Technology Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 114 2024-02-07

Name

Dr. Jasson Samson Rweikiza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza: -

Je, lini Tanzania itajiunga na Mkataba wa Budapest ili kujiimarisha na mapambano dhidi ya makosa ya kimtandao?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jasson Samson Rweikiza, Mbunge wa Bukoba Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkataba wa Budapest ni Mkataba ulioandaliwa mwaka 2001 na Baraza la Umoja wa Ulaya kwa ajili ya Makosa ya Mtandao. Mkataba huu ulianza kufanya kazi Julai Mosi mwaka 2004 na hadi sasa ni nchi 66 kutoka maeneo tofauti duniani ambazo zimejiunga na Mkataba huo, ambapo kati ya nchi hizo nchi 12 ni kutoka Bara la Afrika. Tanzania si miongoni mwa nchi ambazo zimejiunga na Mkataba huo. Aidha, katika hatua ya kutunga Sheria ya Makosa ya Mtandao ya mwaka 2015 kwa sehemu kubwa maudhui ya Mkataba wa Budapest yametumika, kwa kuwa yanaakisi kwa mapana na usahihi mazingira ya kisheria dhidi ya uhalifu wa kimtandao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa kuna jitihada za kuandaliwa kwa Mkataba wa Umoja wa Mataifa dhidi ya makosa ya mtandao ambao unahusisha nchi zote duniani na una mawanda mapana kuliko Mkataba wa Budapest. Hivyo, baada ya kufanya tathmini tumebaini kuwa hakuna haja ya Tanzania kujiunga na Mkataba wa Budapest na badala yake tutajiunga na Mkataba wa Umoja wa Mataifa dhidi ya Makosa ya Mtandao utakaokuwa tayari kuanzia mwaka 2025.