Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 9 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 134 2023-11-09

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: -

Je, lini Serikali itamaliza tatizo la kukatika kwa umeme katika Manispaa ya Morogoro?

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Christine Gabriel Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia TANESCO imechukua hatua mbalimbali katika kutatua changamoto ya kukatika kwa umeme katika Manispaa ya Morogoro, ikiwa ni pamoja na kufunga transformer yenye ukubwa na uwezo wa MVA 120 katika Kituo cha Msamvu. Kazi hiyo ambayo inagharimu jumla ya shilingi bilioni 10.5 inatarajiwa kukamilika mwezi huu wa Novemba, 2023. Aidha, sambamba na hilo, TANESCO inaendelea na ukarabati wa miundombinu ya usambazaji wa umeme katika Manispaa ya Morogoro ili kuondoa tatizo la kukatikakatika kwa umeme katika Manispaa ya Morogoro, ahsante. (Makofi)