Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 47 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 417 2022-06-20

Name

Yustina Arcadius Rahhi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YUSTINA A. RAHHI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha uwekaji wa samani na vifaa vya kufundishia katika Vituo vya Rasilimali za Kilimo?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Yustina Arcadius Rahhi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ilijenga Vituo vya Rasilimali za Kilimo vya Kata 289 katika Halmashauri 184 kati ya mwaka 2007 na 2011. Kwa mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali imeanza uwekaji wa samani na vifaa vya TEHAMA kwa ajili ya kufundishia katika vituo hivyo na kwa mwaka huu wa fedha Wizara itawezesha Vituo 34 vya Halmashauri 27 za Mikoa ya Dodoma, Singida, Morogoro, Tabora, Simiyu, Mwanza, Geita, Lindi, Mtwara, Mbeya, Songwe na Iringa. Kwa ufupi, Wizara itaendelea kuweka samani na vifaa vya kufundishia katika Vituo vyote vya Rasilimali za Kilimo vya Kata vilivyojengwa nchini na kutumika kama Centre of Excellence.