Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 47 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 414 2022-06-20

Name

Abdulhafar Idrissa Juma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtoni

Primary Question

MHE. ABDUL-HAFAR IDRISSA JUMA aliuliza: -

Je, ni lini majimbo ya Zanzibar yatapata fedha za Mfuko wa Jimbo kwa wakati?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Abdul-Hafar Idrissa Juma, Mbunge wa Mtoni, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, fedha za Mfuko wa Jimbo kwenda Majimbo ya Zanzibar hupelekwa kwa wakati na kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za fedha, ambapo fedha hizo huamishwa moja kwa moja kutoka Wizara ya Fedha na Mipango ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenda Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Aidha, katika mwaka 2021/2022 fedha za mfuko kiasi cha Shilingi Bilioni 1.4 zimeshatolewa kwa ajili ya Majimbo ya Zanzibar. Ahsante.