Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 1 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 3 2023-10-31

Name

Edwin Enosy Swalle

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kupeleka Watumishi, Vifaa Tiba na Tendanishi kwenye Vituo vya Afya na Zahanati katika Jimbo la Lupembe?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Edwin Enosy Swalle, Mbunge wa Jimbo la Lupembe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali imetenga shilingi milioni 700 kwa ajili ya ununuzi wa vifaatiba kwa ajili ya hospitali, vituo vya afya na zahanati katika Halmashauri ya Wilaya ya Njombe.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 na 2022/2023, Serikali imepeleka jumla ya watumishi 72 wa Kada mbalimbali za afya kwa ajili ya kutoa huduma katika Halmashauri ya Wilaya ya Njombe.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutenga bajeti ya ununuzi wa vifaa tiba pamoja na kuajiri watumishi wa kada mbalimbali za afya kwa ajili ya kwenda kutoa huduma kwenye vituo kote nchini, ahsante.