Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 1 Youth, Disabled, Labor and Employment Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu 1 2023-10-31

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI K.n.y MHE. STELLA I. ALEX aliuliza:-

Je, upi mkakati wa Serikali kufanya Marekebisho ya Sheria Na. 9 ya mwaka 2010 ya Watu Wenye Ulemavu?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCHAL P. KATAMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, awali ya yote nikushukuru na kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa nafasi hii, lakini uniwie radhi kwamba nataka kutumia fursa hii kukupongeza sana, kwa kuwa Rais wa Mabunge Duniani, hii inadhihirisha uwezo mkubwa lakini weledi mkubwa ulionao katika kuongoza Bunge letu lakini pia kuaminika katika Dunia.

Mheshimiwa Spika, pia nimpongeze sana Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kukupa fursa hiyo lakini zaidi pia kuweza kuwezesha jambo hili kufanikiwa. Haya ni mafanikio makubwa kwa nchi yetu na kwamba, imekuwa kielelezo wewe pamoja na Dkt. Samia Suluhu Hassan cha kufanya sasa leadership tourism katika nchi yetu ya Tanzania, wanaweza kuja kujifunza masuala ya uongozi kupitia Dkt. Samia Suluhu Hassan pia uongozi wako mzuri.

Mheshimiwa Spika, mimi najivunia kuwa wa kwanza kujibu swali leo mbele ya Rais wa Mabunge Duniani. Hili siyo jambo rahisi, najivunia sana hilo lakini pia ni Mbunge wa kipekee kwa sababu hata Waziri Mkuu wa Uingereza anatoka Jimboni kwangu, kwa hiyo ahsante kwa kuniongezea rekodi.

Mheshimiwa Spika, baada ya hayo naomba nijibu swali kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu la Mheshimiwa Stella Ikupa Alex, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Mkakati wa Serikali kwa sasa ni kufanya mapitio ya Sera ya Taifa ya Maendeleo na Huduma kwa Watu wenye Ulemavu ya mwaka 2004 ambapo utekelezaji wake umeanza. Baada ya kukamilika kwa mapitio ya Sera ya mwaka 2004, ndipo hatua za Marekebisho ya Sheria ya Watu wenye Ulemavu (Na. 9) ya mwaka 2010 itaanza kwa kuzingatia mapungufu yatakayobainishwa katika tathmini ya utekelezaji wa Sera ya mwaka 2004. Ahsante.