Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 47 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 411 2022-06-20

Name

Dr. Joseph Kizito Mhagama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Madaba

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya kutengeneza barabara ya Wino hadi Ifinga ambayo wakati wa masika haipitiki?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Kizito Mhagama, Mbunge wa Jimbo la Madaba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini kwa maana ya TARURA, Halmashauri ya Wilaya ya Madaba, imekuwa ikitenga fedha kwa ajili ya kuboresha barabara ya Wino – Ifinga yenye urefu wa kilomita 57 ili iweze kupitika majira yote ya mwaka.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2020/2021 barabara ya Wino – Ifinga ilitengenezwa jumla ya kilomita 21 kwa kiwango cha changarawe kwa gharama ya Shilingi Milioni 398.00 na katika mwaka wa fedha 2021/2022 jumla ya kilomita 15 zimejengwa kwa kiwango cha changarawe kwa gharama Shilingi Milioni 360.46.

Mheshimiwa Spika, mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali imetenga Shilingi Milioni 380.00 kwa ajili ya kujenga kilomita 10.5 kwa kiwango cha changarawe na ujenzi wa maboksi kalavati matatu. Serikali itaendelea kuboresha Miundombinu ya barabara za Halmashauri ya Wilaya ya Madaba kulingana na upatikanaji wa rasilimali fedha.