Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 3 Water and Irrigation Wizara ya Maji 35 2023-11-02

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO aliuliza:-

Je, kwa nini Serikali ilivunja Mradi wa Maji wa KAVIWASU katika Mji wa Karatu bila kuwashirikisha wananchi?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, Ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cecilia Daniel Paresso, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Sheria ya Maji Namba 5 ya mwaka 2019 ya Usambazaji wa Maji na Usafi wa Mazingira kupitia kifungu Na. 13(1)(b) vyombo vya watumia maji vinaruhusiwa kutoa huduma za maji kwa wananchi katika maeneo mbalimbali nchini ambapo chombo cha watumia maji cha KAVIWASU kilikuwa kinatoa huduma kwenye baadhi ya maeneo ya Mji wa Karatu.

Mheshimiwa Spika, katika kuboresha huduma ya maji kwenye Mji wa Karatu, Serikali iliunganisha vyombo viwili vya kutoa huduma ya maji vya KARUWASU na KAVIWASU kuwa chombo kimoja ambacho mpaka sasa kimeendelea kutoa huduma ya maji kwa ufanisi katika eneo lote la Mji wa Karatu. Uundaji wa chombo hicho ulishirikisha wananchi ambapo Wizara ilifanya majadiliano ya kina na Mamlaka za Serikali, Wawakilishi wa Wananchi wa Karatu na wadau wa maji na kufikia maamuzi ya kuviunganisha vyombo hivyo viwili ili kiwepo chombo kimoja madhubuti kitakachosimamia utoaji wa huduma endelevu na kuondoa mkanganyiko wa bei za huduma.