Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 3 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 33 2023-11-02

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza: -

Je, upi mkakati wa kuwapa Wananchi ardhi mbadala wanapoondolewa kwenye maeneo yao kupisha uhifadhi na miradi ya mkakati?

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Answer

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. John Danielson Pallangyo, Mbunge wa Arumeru Mashariki, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni dhahiri, kunakuwepo na ulazima wa wananchi kuachia ardhi pale ardhi inapohitajika kwa matumizi ya umma. Mahitaji hayo ni pamoja na ardhi ya uhifadhi na ardhi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya kimkakati.

Mheshimiwa Spika, mfumo wa sheria nchini, umeweka wazi juu ya takwa na haki ya wamiliki wa ardhi kulipwa fidia ya ardhi na maendelezo pale ardhi inapotwaliwa kwa matumizi ya umma. Aidha, sheria inaruhusu fidia hiyo kulipwa kwa fedha taslimu au kupatiwa ardhi mbadala. Pamoja na sheria kuruhusu wananchi kupewa ardhi mbadala pindi ardhi yao inapotwaliwa, wananchi wamekuwa wakipendelea fidia ya fedha badala ya ardhi mbadala ili kuwawezesha kutafuta maeneo mengine wanayoyahitaji. Ahsante.