Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 3 Health and Social Welfare Ofisi ya Rais TAMISEMI. 30 2023-11-02

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER L. MIDIMU aliuliza:-

Je, lini Serikali itajenga Kituo cha Afya katika Kata za Luguru na Sawida Wilayani Itilima?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Lukago Midimu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na ujenzi wa vituo vya afya katika kata za kimkakati zenye idadi kubwa ya watu na umbali mrefu kutoka kituo cha karibu cha huduma.
Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha mwaka wa fedha 2021/2022 hadi Septemba 2023, jumla ya vituo vya afya 348 vimejengwa nchini kote. Kazi ya ujenzi huu ni endelevu hivyo tathmini ya vigezo kwa Kata za Luguru na Sawida itafanyika na kuingizwa kwenye mipango ya ujenzi, ahsante.