Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 38 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 336 2022-06-06

Name

Eng. Ezra John Chiwelesa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA K.n.y. MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga Jengo jipya la Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Engineer Ezra John Chiwelesa, Mbunge wa Jimbo la Biharamulo Magharibi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo, mwezi Februari, 2022 iliwasilisha maombi maalum ya shilingi bilioni 3.475 kwa ajili ya ujenzi wa jengo la utawala la Halmashauri. Maombi hayo yaliwasilishwa nje ya muda ambapo ukomo wa bajeti kwa mwaka 2022/2023 ulikuwa umeshatolewa hivyo kushindwa kutengwa kwa bajeti hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali katika mwaka wa fedha 2022/2023 itatenga kiasi cha shilingi bilioni 2.7 kwa ajili ya ujenzi wa jengo la utawala la Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo kwa kuwa ni kiasi ambacho kimewekwa na Wizara kwa ujenzi wa majengo ya Halmashauri. Ahsante.