Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 3 Questions to Prime Minister Maswali kwa Waziri Mkuu 2 2024-02-01

Name

Dr. Josephat Mathias Gwajima

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Kawe

Primary Question

MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniruhusu kuuliza swali moja. Tumekuwa na tatizo sugu la upungufu wa walimu wa masomo ya sayansi katika Shule za Sekondari na huu wimbo umekuwa wa muda mrefu sana: Je, ni nini sasa mkakati wa kudumu wa Serikali, kuondoa upungufu wa walimu wa masomo ya sayansi katika shule za Sekondari?

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Baba Askofu, Mheshimiwa Gwajima, Mbunge wa Kawe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba vilevile tunao upungufu wa walimu wa masomo ya sayansi kwenye Shule zetu za Sekondari. Tunapoelekea kutekeleza Sera hii mpya ya Elimu, eneo hili tumeliangalia. Tumeanza kuimarisha ufundishaji wa masomo ya sayansi kutoka Shule za Msingi na kuelekea Sekondari na kuhakikisha kuwa tunapata wafaulu ambao pia na wao tunawapeleka kwenye Vyuo vya Ualimu ili kupata taaluma ya ufundishaji wa masomo ya sayansi tuweze kupata walimu ambao watakuja kufundisha tena elimu hii kuanzia ngazi zote za msingi na sekondari ili tuweze kuongeza idadi hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa, mkakati uliopo ni ule ambao nimeueleza awali kwamba kupitia vibali tunavyopata kutoka kwa Ofisi ya Rais, tunatoa nafasi zaidi ya ajira za walimu wa masomo ya sayansi. Kwa mfano, ajira ya mwisho ya walimu 4,000, nafasi 2,500 zilikuwa za walimu wa masomo ya sayansi na nafasi 1,500 zilikuwa za walimu wa masomo ya Arts. Kwa hiyo, hii ilikuwa inatoa mwanya kwa mwalimu yeyote aliyehitimu mafunzo ya ualimu wa masomo ya sayansi kupata ajira ili kuongeza nguvu ya ufundishaji kule kwenye shule zetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, mkakati huu utaendelea na utakuwa endelevu. Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa pamoja na Wizara ya Elimu wanaendelea kusimamia hili kwa karibu ili kuondoa upungufu mkubwa uliopo kwenye masomo ya sayansi, ahsante sana.

Additional Question(s) to Prime Minister