Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 23 Questions to Prime Minister Maswali kwa Waziri Mkuu 8 2023-05-11

Name

Eng. Ezra John Chiwelesa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi pia na mimi nimuulize Mheshimiwa Waziri Mkuu swali. Mheshimiwa Waziri Mkuu ni sera ya nchi yetu kwamba watu wanapotimiza umri wa miaka 18 wana-qualify kupata Vitambulisho vya Taifa. Tumeona hata kwenye Sensa iliyopita idadi ya Watanzania imeongezeka.

Mheshimiwa Spika, tunajua kwamba kuna watu kipindi kile wanaaandikisha kwa mara ya kwanza wame-qualify na umri umeongezeka na hawajaandikishwa. Pia baadhi ya maeneo ya pembezoni mwa nchi hii wananchi walio wengi hawakupata fursa ya kuandikishwa kwenye ile round ya kwanza. Kwa hiyo wengi wamekaa bila vitambulisho ilhali vitambulisho ni requirement kubwa ambayo inatumika katika kila eneo sasa hivi ambalo wananchi wamekuwa wanahusushwa.

Je, hamuoni kwamba ipo haja ya Serikali kuanza mchakato huu upya kama tulivyofanya kipindi kile cha mwanzo ili Watanzania wengi waliofikia fursa hii iweze kuwapata na hatimaye wapate fursa kama Watanzania wanzao walio na vitambulisho wanavyoendelea kunufaika?

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Chiwelesa Mbunge wa Biharamulo kama ifatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali yetu inaendelea na zoezi la utoaji wa vitambulisho kupitia taasisi yetu ya NIDA. Sote tunafahamu, kwamba tulipoanza kutoa vitambulisho hivi tulipitia hatua kadhaa, na hatua hizi zimekuwa na mafanikio lakini pia changamoto. Awali tulikuwa na idadi ndogo sana ya watumishi kuwafikia wananchi kwa ajili ya kutoa vitambulisho kwenye maeneo yao.

Mheshimiwa Spika, mkakati wa Serikali ni kumwezesha Mtanzania kupata vitambulisho mpaka akiwa kijijini kwake. Sasa tumeongeza idadi ya watumishi na nashukuru Mheshimiwa Mbunge ameipongeza Serikali kwa mafanikio kuwa idadi ya wanaopata vitambulisho imeongezeka Lakini bado kuna maeneo kadhaa.

Mheshimiwa Spika, mimi nimefanya ziara biharamulo na Mkoa wa Kagera kwa ujumla nimepita pia Kigoma lakini pia kule Mkoani Arusha maeneo ya Longido kumekuwa na
changamoto ya watu wetu kadhaa kutopata vitambulisho kwa haraka. Nirudie tena. hapa niliwahi kupata swali hili na nikalijibu; nirudie tena kueleza kwamba inawezekana kabisa wale ambao bado hawajafikiwa na hasa wa mikoa ya pembezoni ni kuwepo kwa chngamoto ya mwingiliano na mataifa ya jirani.

Mheshimiwa Spika, kwa sababu kitambulisho hiki ni cha Taifa, tunapozungumzia kitambulisho cha Taifa tunazungumzia Usalama wa Taifa letu. Tusingependa kitambulisho hiki kila mmoja awe nacho kwa sababu kitambulisho hiki ni kwa ajili ya Watanzania. Sasa pale ambako tunapakana na nchi jirani umakini unaongezeka ikiwemo na idadi ya staff ambao wanaweza kufanya kazi hiyo; na mkakati wetu kukamilisha kwa haraka sana.

Mheshimiwa Spika, Sasa hivi tumeimarisha tumepata mashine mpya. Nilipata nafasi ya kwenda nchini Korea na Mtendaji Mkuu wa NIDA kuzungumza na taasisi ambazo zina- supply machines na tulishapata mashine za kutosha vitambulisho vinatolewa. Kwa hiyo tutawafikia Watanzania katika kipindi kifupi kwa au kuwapa namba kwanza tukichapa vitambulisho au kuwafikia na vitambulisho vyenyewe moja kwa moja, kwa sababu pia Serikali tumerahisisha Watanzania ambao bado wanachelewa kupata vitambulisho basi wapewe namba na hiyo namba itumike kwenye mahitaji yao popote pale.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Waheshimiwa Wabunge wote ambao kwenye maeneo yao kuna tatizo hili la upatikanaji wa vitambulisho kwa haraka sana kwa wananchi kwamba Serikali tumejipanga vizuri taasisi yetu ya NIDA imejipanga vizuri na sasa kasi inaongezeka kwa sababu tumeongeza watumishi ambao wanawafikia wananchi kwenye vijiji ambao tumewaweka kwenye wilaya zetu zote. Pale ambapo kutakuwa na tatizo kubwa sana tunawaruhusu wakati huu tukiwa hapa Bungeni mje mtupe taarifa ya maendeleo ya utoaji wa vitambulisho kwenye maeneo yenu. Niwahakikishie tena kwamba kitambulisho hiki kitamfikia kila Mtanzania na si vinginevyo; na tushirikiane katika kuhakikisha kwamba kitambulisho hiki wanokipata ni Watanzania tu kwa sababu suala la kitambulisho nirudie tena ni Usalama wa Taifa letu.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Additional Question(s) to Prime Minister