Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 23 Questions to Prime Minister Maswali kwa Waziri Mkuu 7 2023-05-11

Name

Kunti Yusuph Majala

Gender

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru na mimi kwa kunipatia nafasi ili niweze kumuuliza Mheshimiwa Waziri Mkuu swali.

Mheshimiwa Spika, kupitia sera ya Serikali kupitia Wizara ya Habari na Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kutoka kwenye mfumo wa analogia kwenda kwenye mfumo wa kidigitali, kwa kutekeleza sera hiyo Serikali imeamua kwa kuanza kwenye mfumo wa malipo kutaka wananchi kuanza kulipa kwa njia ya kielektroniki lakini mfumo huu umekuwa na changamoto kubwa sana ya makato makubwa lakini pia na mawasiliano pia mtandao kutokuwa sawa. Sasa swali langu;

Je, ni nini mkakati wa Serikali moja kupunguza makato lakini pili kuhakikisha inaboresha mfumo wake ili mfumo uweze kufanya kazi kwa uthabiti ili kuondokana na kadhia kubwa ambayo Watanzania wanaipata kwa namna ambavyo jinsi mtandao huu unavyofanya kazi?

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kunti Mbunge Mkoa wa Dodoma kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, uko ukweli kwamba Tanzania kutokana na maendeleo ya tehema na sisi tumeanza kutekeleza mifumo mbalimbali kwa ajili ya kurahisisha utendaji kazi ndani ya Serikali, ikiwemo na ukusanyaji wa mapato kwa mfumo wa kielektroniki.

Mheshimiwa Spika, Tananzia ni moja kati ya nchi ambazo zinaanza siku za hivi karibuni kutekeleza mifumo mbalimbali kielektroniki. Tunapitia katika nyakati kadhaa za mafanikio lakini pia changamoto tunapoelekea kujiimarisha. Ukusanyaji wa mapato yetu kielektroniki ni mfumo ambao unaendelea vizuri sasa pamoja na hizo changamoto. Sasa, ili kukabiliana na changamoto hizi yako maelekezo thabiti yaliyofikiwa na serikali yetu kupitia Rais wetu Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Mheshimiwa Spika, moja ameanzisha Wizara maalumu inayoshughulikia Habari Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kwa lengo la kufanya mapitio ya kina kwenye mifumo hii na kuimarisha tehama hapa nchini, na kusimamia kampuni zote za taasisi na sekta binafsi ambazo zinajishughulisha na mawasiliano ili kuimarisha mifumo hii ya mawasiliano. Kwa hiyo kuna tozo kuwa kubwa lakini pia kuna mtandao kutofanya kazi vizuri suala la tozo hili ni wale walioamua tozo hiyo kuwepo. Haya tunayafanyia kazi, na tumewasikia Waheshimiwa Wabunge mara kadhaa na wananchi pia kuitaka Serikali ipitie makato mbalimbali au tozo mbalimbali ambazo zinazotozwa kwenye maeneo mbalimbali, hilo linafanyiwa kazi.

Mheshimiwa Spika, suala la mtandano hili Mheshimiwa Waziri wa Habari Mawasiliano na Teknolojia ya Habari atakuja mbele yetu Waheshimiwa Wabunge kuja kuwasilisha mpango
wa bajeti, mpango wa kazi ambao tutaufanya mwaka ujao na kuomba ridhaa ya fedha. Moja kati ya mambo ambayo nitamwagiza hapa ni kuja kueleza nini wizara inafanya katika kuimarisha mifumo ya mawasiliano na hasa hii mitandao kuwa imara bila kukatika. Kwa sababu hata pia upande wa Serikali tunapata hasara sana lakini baadhi ya watu ambao wanapata vitendea kazi vya kielektroniki kwa kuzima na kusingizia kwamba mtandao haupo na kujipatia mapato, pia Serikali tunapata hasara.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo tunataka tuimarishe eneo hili ili tuwe na mfumo mzuri wa mtandao kupitia taasisi zetu zinazofanya kazi ya kusambaza mitandao lakini pia Serikali inaimarisha tozo mbalimbali ili kuleta unafuu kwa Watanzani.

Mheshimiwa Spika, malengo yetu tunapokwenda kwenya maendeleo ya tehama tuwe na tehama ambayo inaweza kumhakikishia mtanzania kuitumia katika shughuli zake binafsi na hiyo ndio mwelekeo wetu.

Mheshimiwa Spika, hayo ndio maelezo ya eneo hili ahsante sana. (Makofi)

Additional Question(s) to Prime Minister