Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 23 Questions to Prime Minister Maswali kwa Waziri Mkuu 2 2023-05-11

Name

Florent Laurent Kyombo

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO: Mheshimiwa Spika, nishukuru kwa nafasi.

Mheshimiwa Waziri Mkuu, tumeona Serikali imeonesha nia njema ya kuboresha utoaji wa mikopo ya asilimia 10 ambayo inatokana na halmashauri kwa kufanya maboresho ambayo yatafanya sasa mikopo hii itolewe kwa tija.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri Mkuu, mikopo hii inatolewa katika makundi ya wananwake, vijana na makundi ya watu wenye ulemavu. Mheshimiwa Waziri Mkuu, Vijana inapofika miaka 35, vijana wa kike wana–qualify kuendelea na mikopo hiyo kwa sababu wanakuwa ni wananwake lakini vijana wa kiume mikopo hiyo husitishwa.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri Mkuu, katika maboresho haya mazuri yanayofanyika sasa hivi, Serikali haioni sasa kuna haja ya kuboresha eneo hilo kuingiza kundi la wanaume ambao kimsingi ni wapambanaji wa kiuchumi ili sasa makundi hayo yote manne, wanaume, wanawake, vijana na watu wenye ulemavu waweze kupata mikopo hii waweze kuinua uchumi wao? Mheshimiwa Waziri mkuu nakushukuru. (Makofi)

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kyombo, Mbunge wa Nkenge kule Misenyi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tunayo mifuko ya mikopo ikiwemo na huu wa asilimia 10 uliopo chini ya halmashauri. Mifuko hii imetoa fursa ya wale wanaohusika wanaoweza kuingia kwenye masharti ya mfuko huo kupata mikopo. Mkopo wa asilimia 10 unaosimamiwa na halmashauri kupitia mapato ya ndani umeainisha na kuwalenga zaidi wanawake, vijana na walemavu. Sawa, wanawake, vijana na walemavu haijatamka wanaume lakini kwenye category ya vijana tuna wanaume pale lakini ni vijana. Hata hivyo, haikuwabagua wanaume kwa sababu sio mfuko pekee unatoa mikopo hapa nchini.

Mheshimiwa Spika, tuna mifuko mingi ambayo pia inatoa mikopo kwa wote. Hata hivyo Serikali inafanya jitihada za kutoa fursa kwa yeyote yule awe mwanamke, mwanaume, kujana lakini pia wenye mahitaji maalum kupitia taasisi za fedha.

Mheshimiwa Spika, tuna NMB, CRDB, NBC, AZANIA na mabenki mengine yote ikiwemo Benki ya Kilimo ina fursa ya kwenda kukopa. Kwa hiyo, tunapoona eneo hili huna nafasi nalo nenda kwenye chanzo kingine. Nataka nifike Misenyi nione unaposema unaona vijana wanapewa wanawake tu na wavulana hawapewi sasa nataka tuone ni nini kinachotekelezwa kule Misenyi kwa sababu sisi tunaposema vijana ni wale wa kike na wa kiume wote wakapate mikopo. Kwa hiyo, naona fursa hii tunayo.

Mheshimiwa Spika, kwanza nataka niagize kwenye halmashauri, nirudie agizo langu la kwamba mapato ya kuanzia Aprili, Mei na Juni robo ya mwisho wa mwaka wa fedha, mapato haya yasikopeshwe kwanza tunataka kuyawekea utaratibu mzuri ambao pia unaondoa dosari kama hizo ambazo zinaonekana na zimejitokeza kwenye halmashauri zetu.

Mheshimiwa Spika, tutatoa kauli tukiwa katika kipindi hiki hiki cha Bunge kwa mapato haya ya mwezi nne, wa tano na wa Sita ili tupate mfu,mo mzuri zaidi. Kama kuna ushauri tunaupokea, je, fedha hizo tutumie utaratibu upi katika kukopesha na ziende kwa maeneo yapi yanayoweza kufikiwa kwa haraka zaidi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kwamba tunaendelea kupanua wigo wa maeneo ya kupata mitaji kwa makundi yetu mbalimbali wanaume kwa wanawake, wazee, vijana ili waweze kusimamia miradi yao na eneo hilo liwe kama sehemu ya kupata mitaji. Ahsante sana. (Makofi)

Additional Question(s) to Prime Minister