Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 3 Questions to Prime Minister Maswali kwa Waziri Mkuu 2 2023-02-02

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu.

Mheshimuwa Waziri Mkuu kwa kuwa changamoto hii ya Walimu kuchapa watoto bila utaratibu na tena kikatili, nini sasa Serikali haioni kama kuna haja ya kuwaelimisha Walimu hawa somo la maadili la namna ya malezi ya watoto na makuzi katika shule zetu za Msingi na hata Sekondari?

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Lemburis, Mbunge wa Arumeru kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, taasisi zote za elimu zina taratibu zake, na uendeshaji wa elimu nchini una sheria na kanuni zake ambazo zimewekwa, na ndizo zinazosaidia kuongoza wakuu wa taasisi na wale watumishi wa taasisi husika katika kuzingatia sheria na kanuni zilizowekwa; na ndiyo sababu unaona mambo yanaenda vizuri. Hiyo ni kuanzia elimu ya awali, ya msingi, sekondari mpaka elimu ya juu.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo uainishaji wa sheria hizi na kanuni ndio unaoongoza watumishi walio kwenye sekta hiyo au taasisi hiyo kufuata. Ndiyo maana tunaona sasa utulivu upo na kazi zinaenda kwa sababu kila mmoja anazingatia sheria na kanuni zilizopo. Kwa hiyo hatuwezi kusema tutachukua hatua kali kwa sababu miongozo ipo pale ambapo mtumishi anakiuka taratibu na sheria, sheria ile imeelekeza na adhabu ambazo zinatolewa kwa mhusika. Kwa hiyo utaratibu huo unatumika kama ni adhabu ndogo kwa aliyekiuka utaratibu umeainishwa, kama ni adhabu kubwa imeainishwa lakini pia hata akitakiwa kwenda mahakamani imeainishwa.

Mheshimiwa Spika, lakini tuzingatie tu kwamba taaluma ya ualimu ina misingi yake na imewekea utaratibu pia chini ya Wizara ya Elimu na kwa hiyo zipo kamati za maadili mioongoni mwa walimu. Wakati mwingine vyama vya wafanyakazi kama vile CWT yenyewe inachukua nafasi pia kukaa na walimu kuwafanyia counselling pia kuwaelimisha ili kufanya mambo yanavyokwenda kama utulivu ambao sasa upo na utaratibu huo ndio ambao tunautumia kwa sasa.

Additional Question(s) to Prime Minister