Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Question to Prime Minister

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 53 Questions to Prime Minister Maswali kwa Waziri Mkuu 3 2021-06-17

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. JUSTINE L. NYAMOGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Naibu Spika, taasisi za dini zimekuwa zikikumbwa na adha kubwa, vikwazo vingi na urasimu wakati wa kushughulikia misamaha ya kodi wanapopata vifaa au misaada mbalimbali kutoka nje ya nchi na kusababisha wakati mwingine vifaa hivyo kukaa muda mrefu bandarini na kuingia tena tatizo la storage charges ambazo mwisho wake wanashindwa kuvitoa.

Ni nini kauli ya Serikali kuhusu tatizo hili?

Name

Kassim Majaliwa Majaliwa

Gender

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Answer

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Nyamoga, Mbunge wa Kilolo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeweka utaratibu wa kutoa misamaha kwa baadhi ya taasisi zinazotoa huduma za jamii, zinazolenga kuisaidia Serikali katika utoaji wa huduma hizo. Na misamaha hii ambayo inatolewa inaratibiwa na taasisi zetu zote kama inatoka nje ya nchi inakuja nchini kuanzia mahali pa forodha kama ni bandarini, airport na maeneo mengine taratibu zimeandaliwa vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa suala la urasimu ambalo Mheshimiwa Mbunge amelieleza linatokana pia na wale wenye hizo bidhaa/mali inayoingizwa nchini kwa au kutofuata utaratibu na kuratibu jambo zima bila kufuata utaratibu wake hilo pia nalo linaweza kusababisha kuwa na urasimu wa muda mrefu.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia, bidhaa hizi zinaposafirishwa kutoka nje ya nchi kuingia ndani ili ziweze kupata msamaha, hawa wenye bidhaa hiyo taasisi ya kidini au taasisi yoyote ambayo inapata msamaha ni lazima iwe imeandaa utaratibu wa kupeleka maombi lakini pia kupeleka idadi ya orodha ya mali zinazofuata.

Mheshimiwa Naibu Spika, uzoefu ambao tumeupata Serikalini ni kwamba watu wanaweza kuomba msamaha lakini anachokileta nchini sio kile alichokiombea msamaha. Kwa hiyo, kunakuwa na hatua ndefu ambazo wengine wamesema kwamba hii ni urasimu wa Serikali, hapana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nitoe wito sasa kwa taasisi ambazo zinapata misamaha, kwanza kueleza kikamilifu wanataka kuleta nini ambacho kinatakiwa kipate msamaha lakini bidhaa hiyo inayoletwa kwa misamaha lazima ikidhi matakwa ya Serikali kwamba lazima iende ikatoe huduma ambayo inakusudiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ili kuondoa urasimu ni lazima taratibu hizi zifuatwe mapema ili mzigo unapofika kwenye vituo basi uweze kutoka mara moja. Kwa hiyo, tunaendelea kusimamia taratibu hizi huwa zinakamilka na kwa wito nilioutoa kwa wateja wetu kuhakikisha wanafuata taratibu kwa mapema zaidi ili mzigo unapofika uweze kutoka mara moja. Tumejipanga vizuri na tumetoa maelekezo bandarini, viwanja vya ndege na kwenye mipaka yetu kote nchini ili wateja wetu wapate huduma za haraka sana ikiwemo na wanaopata msamaha.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kutoa majibu hayo kwa Mheshimiwa Nyamoga. (Makofi)

Additional Question(s) to Prime Minister