Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Answers to supplementary Questions by Hon. Dr. Stergomena Lawrence Tax (17 total)

MHE. USSI SALUM PONDEZA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Ningependa nimuulize Mheshimiwa Waziri swali moja la nyongeza kama ifutavyo: -

Mheshimiwa Spika, amenijibu kuwa Serikali ina mpango wa kufanya upimaji na kufanya tathmini. Je, wakati itakapofika kufanya tathmini na upimaji, Mheshimiwa Waziri atakuwa tayari na mimi niambatane naye kwenda kwenye zoezi hilo? (Makofi/Kicheko)
WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Spika, ahsante, Mheshimiwa Mbunge ni mdau wetu na tutakuwa tayari kuongozana naye wakati zoezi hili likiendelea. (Makofi)
MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru naomba kuuliza swali dogo la nyongeza. Wananchi wa Bugosi na Kenyambi kule Tarime Mjini walichukuliwa ardhi yao na Jeshi la Wananchi wa Tanzania tangu 2008, na jeshi hili au Serikali ilifanya tathmini mara ya kwanza 2013, 2017 wakafanya tathmini tena, 2019 na mara ya mwisho na ulitilia mkazo hapa Bungeni walikwenda kufanya uhakiki Juni, 2021 na wakatoa namba ya malipo na wakaahidi kwamba kufikia Agosti, 2021 watakuwa wamelipa lakini mpaka sasa hivi hawajawalipa wananchi hawa.

Mheshimiwa Spika, ningependa kujua ni lini sasa wananchi hawa wa Kenyambi na Bugosi watalipwa fidia zao, ili wapishe Jeshi la Wananchi wa Tanzania waende sehemu zingine kufanya makazi na shughuli za kimaendeleo?
WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Spika, naomba nimjibu Mheshimiwa Esther Matiko kama ifutavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema katika mkakati huo wa miaka mitatu tayari tumeshafanya tathmini na uhakiki katika maeneo yote isipokuwa maeneo ya Zanzibar ambayo ndiyo tutayafanyia quoter hii. Kinachoendelea sasa baada ya huu utathmini ni kufanya uhakiki na uhakiki unaendelea katika maeneo yote ambayo yamefanyiwa tathmini na uhakiki ili tukishakamilisha uhakiki taratibu nyingine zitafuata. (Makofi)
MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni miaka mingi sasa toka ukoloni vijana wetu wanaoajiriwa na Jeshi la Kujenga Taifa wanapewa miaka Sita kabla ya kuolewa au kuoa. Kwa kuwa, magonjwa yamekuwa mengi na kwa kuwa stress za Askari wetu zimekuwa nyingi.

Je, ni lini Serikali itapunguza muda huu wa miaka Sita kuwa miaka Mitatu au Miwil?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, ni muda sasa tunapeleka vijana wetu JKT tunapeleka vijana 2,000 au 1,000 wanachukuliwa labda 50 wanaajiriwa wengine wanarudi nyumbani. Je, ni lini sasa Serikali itakuja na mpango mkakati wa kuandaa vijana wanaorudi nyumbani kuwapa ufundi wa kutosha na saikolojia ili wasiwe panya road? (Makofi)
WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Getere kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaanza kwa kumpongeza kwa kuwa mdau wa karibu wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa na kuwatetea wapiganaji wetu. Swali lake la kwanza ambalo ni kuhusu umri, napenda kwanza nitoe ufafanuzi kwamba ni kweli kwamba Maafisa na Maaskari wenye elimu ya darasa la saba hadi kidato cha sita na wenye Stashahada wao ndiyo hukaa miaka Sita kabla ya kuolewa. Yapo makundi mengine kama wenye shahada ya kwanza wao hukaa kama makapera kwa miaka Minne na wenye Shahada ya Uzamili, wao hukaa kwa miaka mitatu na wenye Shahada ya Uzamivu wenyewe hawana muda wa kukaa kwenye ukapera na hii ni kutokana na aina ya majukumu ambayo maaskari hawa wanafanya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa Askari ambao nimewataja katika kundi la kwanza hao huwa ni vijana wadodo wanajiunga wakiwa na umri wa miaka 18 na kuendelea, kwa hiyo huhitaji kwanza kukomaa. Majukumu ya Jeshi ni majukumu mahususi lakini pia hawa ndiyo wanategemewa kama wapiganaji kwa hiyo huendelea na kozi mbalimbali na kuhakikisha kwamba wako imara wakati wote. Kwa hiyo, miaka hii Sita iliyowekwa imewekwa baada ya kufanya uchunguzi lakini pia kuzingatia vigezo mbalimbali. Kwa hiyo, kama tunaweza kubadilisha sidhani kama hilo linawezekana kwa sasa kwa sababu utafiti ulifanyika na lazima iwe hivyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, hii pia inatokana na aina ya majukumu ambayo wanafanya. Wengine wanapoajiriwa kama Madaktari huenda moja kwa moja kufanya hiyo kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili ambalo linahusiana na vijana wanaokwenda JKT kwamba ni wengi lakini wanaoajiriwa ni wachache. Kwanza ninapenda kueleza kwamba madhumuni ya vijana kujiunga na JKT ni kuwajengea uzalendo, kuwajengea ukakamamu lakini kuwapa stadi mbalimbali ili baada ya hapo waende kujiajiri. Madhumuni siyo kutoa ajira kwa vijana hawa, hilo linafanyika vijana hawa wanafundishwa stadi mbalimbali ili baada ya hapo waweze kujitegemea.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu tuna mpango gani, ni kweli nasi tumeona kwamba pamoja na kuwapa stadi mbalimbali bado kuna umuhimu kuwawezesha vijana hawa kujitegemea. Kwa hiyo, tumeanza kufanya kazi hii na tayari katika mpango wa block farming kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo, tutaona jinsi gani tutaweza kuchukua baadhi ya vijana, lakini bado tunaendelea kulichakata suala hili tuweze kuja na program nzuri zaidi ambazo zitawawezesha vijana hawa kujiajiri baada ya kupata stadi ambazo tunawapatia. (Makofi)
MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Swali la kwanza; kwa kuwa, Waziri amesema tayari mipango ya kufufua Kambi ile inaendelea na sasa hivi hali ya usalama upande wa kusini hasa upande wa Msumbiji sio nzuri katika Vijiji vya Wenje, Lukala, Nasomba, Makandi na Kazamoyo watu hawa wanaishi kwa kutokuwa na amani. Je, haoni sasa ni muhimu kuweka angalau makambi ya temporary ili kurejesha amani ya wananchi wa vijiji hivyo?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa vijiji hivyo kwa sasa ulinzi umekabidhiwa kwa mgambo ambao wako 30 katika vijiji hivyo na wanapewa sh.50,000/= kwa mwezi na Halmashauri.

Je, Serikali haioni sasa ni muhimu kuwalipa mshahara mgambo wale ili waweze kuendelea kulinda mipaka?
WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba nijibu maswali ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua hali ilivyo katika mipaka yetu yote ikiwa ni pamoja na mpaka wa Kusini na tayari hatua mbalimbali zimechukuliwa kuimarisha ulinzi, hatukai tu tukisubiri kambi. Kambi itakuja lakini hatua za kuimarisha ulinzi katika mipaka hiyo zinaendelea na ulinzi umeimarishwa.

Mheshimiwa Spika, swali la pili kuhusu malipo, kwa mgambo kuwa na mishahara upo utaratibu unaotumika kulipa Jeshi la Mgambo na utaratibu huo utaendelea kutumika. Ahsante.
MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Spika, suala hili la Usule limekuwa ni la muda mrefu sana na hii mambo ya uhakiki na hawa akina mama watatu watalipwa fedha zao imekuwa ni muda mrefu sasa. Hebu Serikali itoe majibu ya uhakika, lini hasa hawa wamama watapata fedha zao. (Makofi)

Swali langu la pili, katika Kijiji hiki cha Usule kuna ranch ya Kalunde ambayo Wanajeshi pia walichukuwa maeneo hayo kwenye kaya 14 zaidi ya miaka kumi sasa watu hawa wanaambiwa wamefanyiwa uhakiki lakini hawajalipwa fedha zao. Serikali itoe kauli ya hawa wananchi 14 pia katika ranch ya Kalunde ni lini mtawapa fedha zao ili waende kwenye maeneo mengine waweze kufanya shughuli zao za maendeleo. (Makofi)
WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Spika, ahsante naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge la nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, migogoro ya ardhi ina mchakato na kama unavyoona Mheshimiwa Mbunge mchakato umeshafika ukingoni, tumekwishafanya uhakiki vitabu vimeshaandaliwa na tayari imeshakubalika na fedha zimekwishatengwa. Kwa hiyo, naomba tu Mheshimiwa Mbunge na wananchi wavute subra kidogo ili waweze kulipwa, kwa sababu fedha tayari ziko katika bajeti ya mwaka huu wa fedha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili naomba nilijibu kwamba hii ni kero mpya, kwa hiyo tunaipokea na tutaifanyia kazi na kama itahitajika tutaingiza katika mpango wetu wa kutatua migogoro unaoendelea mpango wa miaka mitatu.

Mheshimiwa Spika, ahsante. (Makofi)
MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Madam Spika, ninakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la dogo nyongeza.

Mheshimiwa Spika, hali iliyoko katika Kijiji cha Usule Mkoani Tabora inafanana kabisa na hali iliyoko Kjiji Tondoroni Wilaya ya Kisarawe, Kata ya Kiluvya Mkoani Pwani, sasa napenda kujua ni lini Serikali mtawalipa fidia wananchi wale au kurudisha yale maeneo ili waweze kuyaendeleza. Ahsante. (Makofi)
WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nitalijibu kwa ujumla nikianza kwa kuwapongeza Waheshimiwa Wabunge wengi ambao wamekwisha niona kufuatilia migogoro ya ardhi katika maeneo yao.

Mhesihimiwa Spika, niseme kwamba tunao mpango wa kusuluhisha hii migogoro baina ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania na wananchi ambao umejumuisha maeneo 152 yanayohusisha Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar. Mpaka sasa tumekwisha pima maeneo 86, tumekwisha fanya uthamini wa maeneo 13 na upimaji unaendelea katika maeneo 66, na mpango huu ni wa miaka Mitatu.

Mheshimiwa Spika, ninaomba baada ya kuwashukuru Waheshimiwa Wabunge wote, maana wengi sana wamekwisha nifuata kwa ajili ya migogoro katika maeneo yao, nawashukuru na kuwapongeza ila niwaombe tu wavute subira tuweze kukamilisha hii michakato inayoendelea. Ahsante.
MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Mgogoro kama huo huko vilevile katika Jimbo la Kigamboni katika Kata ya Kimbiji eneo la Kijaka.

Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro huo.
WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Spika ahsante sana. Naomba nijibu swali la Mheshimiwa Ndugulile kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze sana kwa kulifuatilia suala hili kwa karibu, kwa niaba ya wananchi wa Kigamboni na ninapenda kumfahamisha kwamba mgogoro huu tayari na wenyewe unashughulikiwa na upimaji ulishafanyika, kwa hiyo tunasubiri tupate hati na baada ya hapo hatua zinazofuata zitaendelea. (Makofi)
MHE. SUBIRA K. MGALU: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza mawali mawili madogo ya nyongeza. Kwanza niishukuru sana Serikali yetu ya Awamu ya Sita kwa kuonesha dhamira ya kushughulikia mgogoro huu ambao ulikuwa wa muda mrefu. Sasa kwa kuwa hatua ya kwanza ya kuanza kulipa malipo haya kwa Kitongoji cha Funta zaidi ya milioni 330 imeleta kama sintofahamu kwa wananchi wa Vitongoji vya Chokozeni na Kudikongo katika Kijiji cha Kihangaiko hicho hicho. Je, Serikali haioni ipo haja kwa vitongoji hivi viwili vya Kijiji kimoja cha Kihangaiko walipwe fidia yao kwa mwaka huu wa fedha unaoendelea?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa wapo baadhi ya wananchi waliotoa maeneo wa Vijiji vya Msata, Kihangaiko na Pongwe Msungura hawakupimiwa na kwa kuwa imeanza kulipa fidia. Je, Serikali inatoa tamko gani kwa wale wananchi ambao bado hawajapimiwa ili waweze kupata matumaini na waweze kuyaachia yale maeneo kuliko wanavyokwenda kufanya shughuli na wanakumbwa na matatizo makubwa? Ahsante sana.
WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Spika, kwa swali la kwanza ambalo ni kwamba kuna hawa ambao hawajalipwa, napenda tu kutoa rai kwa wenzetu ambao ni Halmashauri ya Chalinze kukamilisha taratibu na kuwasilisha jedwali ili taratibu ziendelee na ziweze kukamilika. Kama alivyosema ni dhamira ya Serikali kuhakikisha kwamba migogoro hii inakamilishwa na kama ambavyo Waheshimiwa Wabunge wengi wataona tulikuwa na migogoro 87 katika mpango wetu wa mwaka 2020 - 2023 na kati ya migogoro hiyo 87 migogoro 74 imekwishatatuliwa. Kwa hiyo hii 13 iliyosalia ni dhamira yetu kuhakikisha kwamba tunaikamilisha mwaka huu wa fedha kwani hata mpango tuliokuwa tumejiwekea kukamilisha mwaka 2023 umeshapita, tumeongeza mwaka mmoja.

Mheshimiwa Spika, kwa hao wengine ambao wamejitokeza, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaangalia kama hii migogoro mipya iko sehemu ya mpango wetu na kama haiko sehemu ya mpango wetu tutaona tunaiingiza namna gani. Jambo la kwanza ni muhimu tuende tukajiridhishe kwamba haya maeneo anayoyataja ni maeneo ambayo yapo katika maeneo ya vikosi vya Jeshi. Tutafanya hivyo Mheshimiwa Mbunge kwa kushirikiana na wewe.
MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa vile changamoto iliyoko katika Halmashauri ya Chalinze inafanana na changamoto iliyoko katika Halmashauri ya Bagamoyo katika Kata ya Mapinga katika eneo la Kiharaka. Je, Serikali lina mpango gani kulipa wananchi wa eneo la Kiharaka katika Kata ya Mapinga? Ahsante. (Makofi)
WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na naomba nijibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama nilivyokwishasema tunao mpango ambao umejumuisha migogoro mingi, kwa hiyo, kama hili eneo la Kiharaka ni sehemu ya mpango huu basi litakamilishwa katika mpango huu wa fedha, lakini kadri tulivyoendelea kutatua hii migogoro, migogoro mipya pia imekuwa ikijitokeza, kwa hiyo, kama huu ni mgogoro mpya tutaujumuisha katika mpango wetu baada ya kujiridhisha kwamba ni eneo ambalo lina mgogoro na Jeshi, ahsante.
MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Spika, moja kati ya maeneo ambayo yanaleta changamoto ni eneo la Kata ya Tambukareli ambapo ni eneo la Jeshi na kuna makaburi ya wananchi ambayo yapo kwenye eneo la Jeshi.

Je, Serikali mna mpango gani wa kwenda kufanya mazungumzo na wananchi ambao wamezika ndugu zao kwenye maeneo yale ili waweze kuendelea kufanya Ibada kwa marehemu waliotangulia mbele ya haki? (Makofi)
WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Spika, nimshukuru Mheshimiwa Mbunge kwa kuendelea kufuatilia suala hili kwa karibu sana. Hata kabla, huko nyuma tulishazungumza kuhusu suala hili, hili ni miongoni mwa maeneo ambayo yanafanyiwa kazi. Kwa hiyo, nikuhakikishie tu kwamba tutaendelea kulifanyia kazi ili tuweze kupata suluhu yake, ahsante. (Makofi)
MHE. SILVESTRY F. KOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu hayo mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, mali hizo zenye thamani ya takribani shilingi bilioni 37 ni mali ya Chama cha Wazee Waliopigana Vita ya Pili ya Dunia (TLC) ambazo wana haki nazo pamoja na watoto wao kwa mujibu wa katiba yao. Mali hizo zimekodishwa kwa muda mrefu na pesa zinakusanywa, mfano ni Upanga pamoja na kule Tarime, lakini fedha hizo hazijawafikia wale wazee ambao wanaishi kwa shida na wengine wanafariki hata kwa kukosa chakula: Je, ni lini Serikali itahakikisha fedha hizo zinawafikia wazee hao wafaidike nazo?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Kamati ya Serikali iliyokaa kwenye majadiliano mbalimbali haijawahusisha wazee hao wala watoto wao: Je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kupanga siku maalum ambayo atakutana na Kamati ya Wazee na Watoto hao ili washiriki kufikia maamuzi hayo ambayo Serikali imeyafikia?

Mheshimiwa Naibu Spika, nimalizie tu kwa ku-declare kwamba baba yangu pia ni mmoja wa veteran waliopigana Vita ya Pili ya Dunia na sasa hivi ana miaka 103, ana akili timamu na anaulizia sana mali hizo.
WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kama nilivyojibu kwenye swali langu la msingi, tathmini imeshafanyika na sasa tuko kwenye hatua ya kuhakikisha kwamba tunawafidia wazee hawa. Kwa hiyo, hili linaendelea.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu tathmini ya kutowahusisha wazee waliopigana vita na watoto wao, tathmini hii ilikuwa pana na ilihusisha taasisi mbalimbali za Serikali. Bahati mbaya viongozi wa Chama cha TLC wote wamefariki, alikuwa amebaki mmoja wakati tathmini inaanza, lakini naye kwa sasa ameshafariki, hata hivyo tulihusisha baadhi ya familia ambazo tuliweza kuzifikia. Kwa hiyo, tathmini iliwahusisha wadau mbalimbali, nafikiri ikiwa nni pamoja na wewe Mheshimiwa Mbunge, tuliweza kupata mawazo yako kwa nyakati mbalimbali.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.
MHE. KHALIFA MOHAMED ISSA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kuna wanajeshi wengi wastaafu waliopigana tokea baada ya uhuru, wamestaafu na mpaka leo wako hai, lakini pensheni zao za mwezi ni ndogo sana: Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwarekebishia ili waweze kukidhi maisha yao? Ahsante. (Makofi)
WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Ni kweli wapo watumishi wa umma ikiwa ni pamoja na wanajeshi wastaafu ambao wamekuwa wakilalamikia pensheni zao kuwa ndogo. Hili ni suala ambalo linafanyiwa kazi kwa pamoja na sekta nyingine zinazohusika na masuala ya pensheni. Kwa hiyo, tutaendelea kuliangalia na kuona ni jinsi gani linaweza kufanyiwa kazi kwa kuzingatia umuhimu wa kazi ambayo wanajeshi hao walifanya na pia kwa kuzingatia uhalisia wa bajeti ya Serikali yetu, ahsante.
MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Nimshukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu mazuri na niko tayari kuvuta subira kusubiri hiyo tume itakayotuletea majibu ila nilikuwa nina ombi moja kwa Mheshimiwa Waziri, je, tume hiyo itakapomaliza kazi, yuko tayari kwenda na mimi Mbozi kuzungumza na wananchi wa hivyo vijiji na kutoa majibu kwa wananchi hao? Ahsante. (Makofi)
WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kama nilivyokwishamuahidi Mheshimiwa Mbunge, tumeshazungumza suala hili mara nyingi na nathibitisha tu kwamba, niko tayari kwenda kuongea na wananchi wake. (Makofi)
MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri na nimpongeze sana kwa majibu mazuri. Nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza, kama mnavyojua kwamba, baadhi ya Kamandi au Kambi kumekuwa na tabia ya ukataji wa miti na uondoaji wa misitu ambayo imekuwepo kwa muda mrefu. Sasa, nilikuwa naomba tu kujua Mheshimiwa Waziri, wana mwongozo gani wa kushirikiana na Taasisi za Idara za Mazingira na Misitu hasa kule Zanzibar, ili kuona kwamba miradi hii ikiibuliwa na ikitekelezwa basi haiathiri mazingira?

Swali namba mbili, je, Kamandi au Wizara ina utaratibu gani wa kuwa na mwongozo wa mapato na matumizi kama vile walivyo wenzetu wa Jeshi la Polisi ule mpango wa Tuzo na Tozo, ili kuhakikisha kwamba, mapato yanayopatikana yanatumika katika njia ya ufanisi zaidi? Ahsante sana. (Makofi)
WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu kwenye swali la msingi, miradi hii huzingatia pia taratibu za uhifadhi wa mazingira. Kwa hiyo, tunafuata mwongozo wa Serikali kuhakikisha kwamba, taratibu za uhifadhi wa mazingira zinazingatiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Mwongozo wa mapato na matumizi; Miradi hii inaendeshwa kwa kuzingatia kwanza inachambuliwa na Makao Makuu ya Jeshi na umewekwa utaratibu ambao pesa zote zinazopatikana zinafuata Taratibu za Matumizi ya Fedha katika Taasisi za Umma. Kwa hiyo, hakuna wasiwasi kwamba, pesa hizi labda zinapotea na nipende kutoa pongezi kubwa sana kwa Jeshi letu la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania, kwa kazi kubwa mabyo wameifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna kipindi tulikuwa na ukwasi lakini miradi hii imesaidia katika kutekeleza majukumu ya msingi ya Jeshi. Kwa hiyo, nawapongeza sana Jeshi letu na nikuhakikishie kwamba, taratibu na matumizi ya fedha haya yanafuata taratibu zote, hata audit huwa zinafanywa, ahsante sana.
MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri na nimpongeze sana kwa majibu mazuri. Nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza, kama mnavyojua kwamba, baadhi ya Kamandi au Kambi kumekuwa na tabia ya ukataji wa miti na uondoaji wa misitu ambayo imekuwepo kwa muda mrefu. Sasa, nilikuwa naomba tu kujua Mheshimiwa Waziri, wana mwongozo gani wa kushirikiana na Taasisi za Idara za Mazingira na Misitu hasa kule Zanzibar, ili kuona kwamba miradi hii ikiibuliwa na ikitekelezwa basi haiathiri mazingira?

Swali namba mbili, je, Kamandi au Wizara ina utaratibu gani wa kuwa na mwongozo wa mapato na matumizi kama vile walivyo wenzetu wa Jeshi la Polisi ule mpango wa Tuzo na Tozo, ili kuhakikisha kwamba, mapato yanayopatikana yanatumika katika njia ya ufanisi zaidi? Ahsante sana. (Makofi)
WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu kwenye swali la msingi, miradi hii huzingatia pia taratibu za uhifadhi wa mazingira. Kwa hiyo, tunafuata mwongozo wa Serikali kuhakikisha kwamba, taratibu za uhifadhi wa mazingira zinazingatiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Mwongozo wa mapato na matumizi; Miradi hii inaendeshwa kwa kuzingatia kwanza inachambuliwa na Makao Makuu ya Jeshi na umewekwa utaratibu ambao pesa zote zinazopatikana zinafuata Taratibu za Matumizi ya Fedha katika Taasisi za Umma. Kwa hiyo, hakuna wasiwasi kwamba, pesa hizi labda zinapotea na nipende kutoa pongezi kubwa sana kwa Jeshi letu la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania, kwa kazi kubwa mabyo wameifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna kipindi tulikuwa na ukwasi lakini miradi hii imesaidia katika kutekeleza majukumu ya msingi ya Jeshi. Kwa hiyo, nawapongeza sana Jeshi letu na nikuhakikishie kwamba, taratibu na matumizi ya fedha haya yanafuata taratibu zote, hata audit huwa zinafanywa, ahsante sana.
MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina swali moja la nyongeza ambalo linaendena na pongezi kwa Serikali kurejesha mafunzo hayo.

Mheshimiwa Spika, swali langu; je, kwa kuwa vijana wengi wamekuwa na mwitikio mkubwa sana wa kupenda kujiunga na mafunzo ya JKT lakini nafasi hazitoshi kwa wale wa kidato cha sita wanaomaliza na wale wa kidato cha nne ambao wana mafunzo ya ziada kama ya ufundi na kadhalika.

Je, ndani ya mifumo ya Serikali iko tayari kuongezea nguvu Jeshi la Kujenga Taifa ili kila kijana mwenye sifa aweze kupata nafasi hiyo kwa nia ile ile ya kumjengea ukakamavu na uhodari katika utendaji kazi? (Makofi)
WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cosato David Chumi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli mwitikio umekuwa mkubwa na Jeshi la Kujenga Taifa tumekwishaandaa mpango wa utekelezaji utakaowezesha kuwachukua vijana wengi zaidi. Utekelezaji wa mpango huu utatuwezesha kuwachukua vijana wengi lakini pia utategemea upatikanaji wa rasilimali. (Makofi)
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa condition hii ya kupita JKT na Serikali imekiri kwamba uwezo wa kuwachukua watu wote haupo lakini recently tumekuwa tunaona ajira nyingi zinazotangazwa zimeweka kigezo cha kwamba kijana awe amepita JKT. Kwa hiyo vijana wengi wanatamani waingie kwenye hizi ajira lakini kigezo cha kupitia JKT kinawanyima fursa na hawatendewi haki;

Je, hatuoni sasa ni wakati muafaka kwa Serikali kuondoa kigezo cha kupita JKT mpaka pale itakapokuwa tayari kuwahudumia watu wote ili ushindani uweze kuwa sawa?
WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba lalamiko hili limeshasikika, na kama tulifufatilia Taarifa ya Tume ya Jinai ni moja ya mapendekezo yaliyotolewa na ni pendekezo linalofanyiwa kazi na Serikali. (Makofi)