Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Questions from Hon. Furaha Ntengo Matondo (1 total)

MHE. FURAHA N. MATONDO aliuliza: -

Je, lini Bima ya Afya kwa watu wote itaanza kutumika?
NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Furaha Ntengo Matondo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote ilipitishwa na Bunge tarehe 1 Novemba, 2023 na Mheshimiwa Rais ameidhinisha sheria hiyo tarehe 19 Novemba, 2023 na imechapishwa katika gazeti la Serikali la tarehe 1 Desemba, 2023.

Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza maandalizi ya kuanza kutumika kwa Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote ambapo kwa mujibu wa Kifungu cha kwanza cha Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote Waziri anaweza kuteua baadhi ya vifungu vya kuanza kutumika. Baadhi ya vifungu ambavyo vinaweka mifumo imara ya kutekeleza Bima ya Afya kwa Wote vimeainishwa na kuwasilishwa kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Sheria itatangazwa kuanza kutumika kabla ya mwisho wa mwezi wa Aprili, 2024 kwa tarehe itakayotajwa.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.