Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Answers to Primary Questions by Hon. George Ranwell Mwenisongole (1 total)

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza:-

Je, kwa nini Serikali isitumie teknolojia na vifaa vya kisasa kusafisha barabara za TANROADS?

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Esther Nicholas Matiko, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imelichukua wazo la Mheshimiwa Mbunge na itaona ni namna gari nzuri ya kujumuisha teknolojia na vifaa vya kisasa katika kufanya usafi wa barabara pasipo kuathiri ajira za vikundi maalum ambavyo vimesajiliwa na Halmashauri za Miji, Wilaya, Mikoa, Manispaa na Majiji kwa kuzingatia matakwa ya Sheria ya Ununuzi wa Umma ya mwaka 2011 na Kanuni zake za mwaka 2016, ahsante.