Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Questions from Hon. Asya Mwadini Mohammed (1 total)

MHE. ASYA MWADINI MOHAMMED aliuliza: -

Je, kuna viwanda vingapi vya kuchakata taka ngumu nchini?
NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara napenda kujibu swali la Mheshimiwa Asya Mwadini Mohammed, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Tanzania hadi sasa tuna jumla ya viwanda 137 vya kuchakata taka ngumu hapa nchini. Viwanda hivyo vimegawanyika katika makundi manne ambayo ni viwanda vinavyotumia taka zitokanazo na chuma viko 16; viwanda vinavyotumia taka za plastiki viko 70; viwanda vidogo vya kutengeneza mkaa mbadala kutoka kwenye mabaki ya kilimo viko 50; na tuna kiwanda kimoja cha kutengeneza mbolea aina ya mboji inayotokana na mabaki ya vyakula. Nakushukuru.