Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon Toufiq Salim Turky (1 total)

MHE. TOUFIQ SALIM TURKY: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa majibu mazuri ya Serikali na naomba kuuliza swali la nyongeza, tukijua kuwa malighafi nyingi ndani ya nchi yetu inatoka katika vijiji. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhamasisha sekta binafsi waweze kuwekeza hizo industrial pack ili wananchi waweze kunufaika katika Taifa lao hususani kwenye vijiji? Ahsante. (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MIPANGO NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Kituo cha Uwekezaji pamoja na Mamlaka ya EPZA, tumeendelea kuhamasisha wawekezaji kupitia njia za makongamano na forum mbalimbali. Hivi ninavyozungumza wiki iliyopita tu, tulikuwa na wawekezaji wa ndani 200 na wawekezaji kutoka China 100, walikutana pamoja na kuweka mikakati ya kuweza kushirikiana kwenye kuwekeza katika haya makongamano makubwa. Kwa hivyo, niwakaribishe hata Waheshimiwa Wabunge akiwemo Mheshimiwa Toufiq ambaye ni mfanyabiashara muhimu kabisa katika nchi yetu, aweze kuwekeza katika maeneo hayo. (Makofi)