Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

Hon. Zainab Mndolwa Amir

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo

MHE. ZAINAB M. AMIR: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumpongeza Mheshimiwa Mhandishi Dkt. Charles John Tizeba (Mbunge), pamoja na Naibu wako Mheshimiwa Dkt. Mary Mwanjelwa (Mbunge) kwa kazi nzuri mnayoifanya katika Wizara hii ya Kilimo. Naishauri Serikali iongeze idadi ya wataalam mabwana shamba na mabibi shamba ili wawasaidie kutoa elimu ya kutosha kwa wakulima wetu ili waweze kulima kilimo cha kisasa na chenye tija kwa wakulima na Taifa kwa ujumla.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali itoe mbolea na madawa kwa wakati ili iwasaidie wakulima kuweza kuitumia kwa wakati na kuweza kupata mazao bora na mengi kwa chakula na biashara. Serikali iwaruhusu wakulima waweze kuuza mazao nje ya nchi kwa kuzingatia taratibu zilizowekwa na nchi. Naishauri Serikali iwasaidie na kuwawezesha wakulima walime mazao ambayo yatatumika kama malighafi katika viwanda vyetu na kuepuka kuagiza malighafi za viwanda vyetu kutoka nje ya nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali iendeleze kilimo cha umwagiliaji katika Mikoa yote ya Tanzania ili kuweza kupata mazao mengi bila kutegemea mvua ambayo kwa wakati mwingine haina uhakika kutokana na mabadiliko ya tabianchi. Naishauri Serikali skimu iliyopo Wami Dakawa iboreshwe ili kuweza kupata mpunga mwingi kwa kuboresha miundombinu yake ambayo ni ya muda mrefu. Pia kuongeza eneo kutoka hekari zilizopo 2,000 hadi 5,000 ili kuweza kuwapa fursa baadhi ya wakulima wapate eneo linalotumia kilimo cha umwagiliaji badala ya kutegemea mvua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali iwashirikishe wakulima katika upangaji wa bei ya mazao na siyo Serikali kutoa bei elekezi kwa wakulima ambayo wakati mwingine haina tija kwa wakulima kulingana na gharama walizotumia katika kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho namuomba Mwenyezi Mungu Mheshimiwa Waziri pamoja na Naibu wako awape afya njema na umri mrefu ili muweze kuwatumikia Watanzania.