Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Dr. Philip Isdor Mpango

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Na mimi nianze kwa kuwapongeza Mheshimiwa Waziri wa Maji, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na timu yote ya wataalam kwa kazi nzuri wanayoendelea kulifanyia Taifa hili. Nianze kwa kusema naunga mkono hoja. Napenda kuchangia kwa kujibu hoja chache, moja ikiwa ni ile ambayo ilikuwa ina sema ziko wapi fedha za India, ule opo nafuu wa dola milioni 500 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maji katika miji 17.

Mheshimiwa Naibu Spika, fedha hizi zilichelewa kupatikana kwa kuwa Serikali ya India iliendelea kusisitiza kwamba matumizi ya fedha hizi lazima zisamehewe kodi zote, za aina zote wala tozo zinazohusika. Na sisi kwa upande wetu kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania tulisisitiza kwamba kodi stahiki zilipwe kwa mujibu wa sheria na hususan Kodi ya Mapato. Mtakumbuka mwezi Septemba, 2017 Bunge hili lilifanya marekebisho ya Sheria ya VAT ambapo lilimpa mamlaka Waziri wa Fedha kusamehe VAT kwa miradi ambayo inagharamiwa kwa mikopo nafuu na ile ambayo inagharamiwa na wafadhiri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo hili tukalimaliza, nilishauriwa ipasavyo na nikasamehe VAT, lakini zikabaki kodi za mapato, kwa mujibu ya Sheria ya Mapato iliyofanyiwa marekebisho mwaka jana ninaweza tu kusamehe pale tu ambapo nitakuwa nimepata ridhaa ya Baraza la Mawaziri.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo tumefanya hivi na tarehe 15 Aprili Serikali iliridhia kusamehe kodi za mapato. Kwa kifupi kuna withholding tax on interest kwa Exim Bank kwa kiwango cha asilimia 10 ambazo ni takribani shilingi bilioni 24.9. Pia kulikuwa na kodi ya mapato kwa makampuni na wafanyakazi. Kodi ya Mapato peke yake ni takribani dola milioni 30 na kwa wafanyakazi dola milioni 15. Lakini pia kulikuwa na withholding tax on commitment fees kwa Exim Bank ambazo imebidi tusamehe, takriban dola 375,000 na tano elfu. Pia zipo kodi zingine SDL na ushuru wa forodha.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema tarehe 15 Aprili Serikali iliridhia kusamehe pia hizi kodi za mapato, na naomba kulialifu Bunge lako tukufu saa 11 na dakika 27 nimeletewa taarifa na naomba niisome inasema hivi; “Kindly Lebam formed that we have successfully concluded the negations with Exim Bank of India, we will sign the agreement tomorrow morning In Shaa Allah.” (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hii ni taarifa ambayo nimeletewa na kiongozi wa Government Negations Team ambayo iko India kwa ajili ya kumaliza zoezi hili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ambalo ningependa kulisemea kidogo ni lile ambalo limesemwa kwa hisia sana na lilishatolewa azimio na Bunge lako tukufu kwamba Serikali iongeze tozo ya mafuta kutoka shilingi 50 mpaka shilingi 100 kwa lita na hizo zilizokusanywa zipelekwe kutunisha mfuko wa maji na hususani miradi ya maji vijijini.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba tu niseme kwamba Serikali kupitia kikosi kazi cha maboresho ya kodi, inakamilisha uchambuzi wa faida na hasara ya utekelezaji wa agizo hili na tutalitolea taarifa kwa umma na kwa Bunge hili kupitia hotuba ya Bajeti Kuu ya Serikali na uchambuzi ambao tunafanya unahusu mambo mengi.

Kwanza ni pamoja na faida za hatua inayopendekezwa. Lakini pia tunatazama risks zake na ukubwa wake kwa uchumi wa taifa na hili ni muhimu lakini pia kungalia madhara yake na hasa kwa Watu wanyonge wa nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ambalo linafanyika katika uchambuzi huu ni kuangalia vyanzo vingine vya ku-finance maji. Kwa hiyo, ukiaccha huu mkopo wa india ambao nimeshausema, lakini tunaangalia pia mikopo mingine nafuu, na hususani mkopo wa dola milioni 300 ambao tunautaraji kutoka Benki ya Dunia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana naunga mkono hoja.