Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. ENG. RAMO M. MAKANI: Mheshimiwa Naibu Spika, pongezi kwa Wizara, Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu, Wakuu wa Taasisi chini ya Wizara, wataalam, Wenyeviti wa Bodi na kikosi kizima cha Wizara. Majukumu ya Wizara hii ni mengi, makubwa na magumu, tunafahamu, lakini jitihada zenu zinaonekana. Hongereni sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, Shukrani. Nimrona miradi michache ambayo jimbo langu limebahatika kutengewa fedha, baadhi ni ile inaendelea, hususan ule wa huduma ya maji, Tunduru Mjini.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu Mradi wa Maji Tunduru Mjini, tunaomba kasi ya utekelezaji iongezeke ili mradi huu ukamilike haraka iwezekanavyo. Tunaomba ukamilifu wa mradi kwa viwango vya kitaalam.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu Miradi ya Maji Vijijini, hali sio nzuri kwa upatikanaji wa huduma za maji vijijini katika Jimbo langu la Tunduru Kaskazini. Kwa kuanzia, naomba vijiji vifuatavyo vipewe kipaumbele; Nakapanya, Muhunesi, Majmaji, Sisi Kwa Sisi, Cheleweni, Huria, Namwinyu.

Mheshimiwa Naibu Spika, wahandisi, mafundi sanifu na mafundi sadifu; kuna uhaba mkubwa sana wa wataalam katika Wilaya ya Tunduru. Katika hali hii ni vigumu kupata ushauri sahihi kusimamia miradi kwa uhakika na kutekeleza majukumu ya kitaalam. Ushauri huu ni kwa Taifa zima.

Mheshimiwa Naibu Spika, ushirikiano kati ya wataalam wa Halmashauri ya Wilaya na wale wa Mamlaka ya Mkoa au Mhandisi wa Maji wa Mkoa ni vema kanuni na taratibu zilizopo zikaangaliwa upya. Iwapo kuna kasoro za kisera, kisheria, kanuni na taratibu zirekebishwe na iwapo tatizo ni utekelezaji tu basi wahusika wapewe miongozo kwa msisitizo na wale wanaokaidi bila kujali ni mara ngapi wameshauriwa wachukuliwe hatua stahiki.