Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Itifaki ya Nagoya ya Kusimamia Upatikanaji na Mgawanyo Sahihi wa Faida zitokanazo na Matumizi ya Rasilimali za Kijenetiki.

Hon. Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Itifaki ya Nagoya ya Kusimamia Upatikanaji na Mgawanyo Sahihi wa Faida zitokanazo na Matumizi ya Rasilimali za Kijenetiki.

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa hii ya kuwa mchangiaji wa kwanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nianze kwa kuunga mkono itifaki ya Azimio hili na kwa namna ya kipekee kabisa niwaombe Waheshimiwa Wabunge wenzangu tuunge mkono hili jambo muhimu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi natokea Mafia, kwa kiasi kikubwa sana maisha ya watu wa Mafia ambayo ni kisiwa maisha yetu ni bahari na bahari ndio watu wa Mafia. Chochote kile ambacho kinaelekea katika kulinda na kuhifadhi bahari kwa maana nyingine hicho ni chenye kutoa manufaa na nafuu kwa watu wa Mafia. Hali ya mazingira ya bahari kwa sasa ni mbaya sana, kwa maana ya kwamba kuna baadhi ya visiwa, Mafia ni kisiwa lakini ndani yake kuna visiwa vidogo vidogo. Vile visiwa vidogo vidogo vingine vimeshaanzwa kumezwa na bahari kutokana na uchafuzi wa mazingira na mabadiliko ya masuala ya tabianchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tulipokuwa wadogo kule Mafia tulikuwa tunakwenda kuvua katika maji usawa wa magoti, lakini sasa hivi unaweza ukaenda maji ya kina kikubwa kabisa na vyombo na ukarudi ukiwa na kikapu kimoja au pengine ukarudi mikono mitupu. Kwa hiyo, ipo haja ya makusudi kabisa sisi Wabunge tukubaliane na tuliunge mkono Azimio hili ambalo lina nia njema na nchi yetu na mazingira yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, takwimu zinaonesha ifikapo mwaka 2030 ndani ya bahari na hususan Bahari ya Hindi kutakuwa na takataka nyingi zaidi kwa maana ya mifuko hii ya “rambo” na mifuko mingine ya plastiki kuliko samaki wenyewe. Kwa hiyo, hali ni mbaya sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata ilipotokea ile ndege ya Malaysia ikapotea na ikasemekana imeangukia baharini ndipo wataalam wakaenda kugundua mambo makubwa zaidi yaliyokuwepo chini ya bahari kutokana na uchafuzi wa mazingira, wakakuta kuna takataka nyingi mno. Tuna kila aina ya sababu kuhakikisha kwamba tunaunga mkono Azimio hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mafia kuna taasisi maalum inayohusiana na masuala ya uhifadhi wa bahari maarufu kama Marine Park. Ningeomba sana na sina uhakika kama Waziri mwenye dhamana ya Kilimo, Uvuvi na Mifugo yupo hapa, lakini ningeomba sana watusaidie wenzetu wa Serikali kuhakikisha kwamba ile Taasisi ya Hifadhi ya Bahari inajikita na kujiingiza zaidi katika suala la uhifadhi. Kwa sasa hivi wamekuwa wana mambo mengi zaidi kuliko uhifadhi wenyewe. Wamejiingiza katika masuala ya ukusanyaji wa maduhuli, wamejiingiza katika masuala ya ujenzi, masuala ya uwekezaji na uuzaji wa visiwa, wanajikuta mpaka kwenye the core business yao wamekuwa diverted na sasa wanashughulika zaidi na mambo ambayo hayawahusu na hayahusiani zaidi na uhifadhi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba sana kama Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi yupo hapa ahakikishe kwamba, anawaelekeza watu wa hifadhi ya bahari Mafia wajikite kwenye uhifadhi, hiyo ndiyo shughuli yao ya msingi waachane na habari ya kuuza visiwa, kuuza maeneo, mambo ya ujenzi, uwekezaji, ukusanyaji wa maduhuri hilo ni suala la TRA na Halmashauri ya Mafia tunaweza tukayafanya sisi wenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumze kidogo suala la mbadala. Ndugu yangu Mheshimiwa Kitandula amekuwa akizungumza sana hapa, suala la ufugaji wa samaki. Baharini samaki wa bahari pia wanafugwa. Sasa kutokana na hali…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)