Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Julius Kalanga Laizer

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Monduli

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. JULIUS K. LAIZER: Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iwalipe wananchi fidia ambao mazao yao yaliharibiwa na tembo katika maeneo ya Mswakini, Makuyuni, Lokisala, Lemooti na Monduli Juu. Pia ni lini Serikali italipa fedha za WMA zinazodaiwa na WMA ya Randilen? Ni muhimu Wizara hii ikarejesha fedha hizo kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Monduli imezungukwa na Mbuga za Ngorongoro na Tarangire tunaomba Wizara ione namna ya kutupatia gari la doria ili kunusuru mazao na maisha ya watu wetu.