Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. John John Mnyika

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Kibamba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kufuatia kugawanywa kwa Manispaa ya Kinondoni na kuanzishwa kwa Wilaya mpya ya Ubungo, Hospitali ya Mwananyamala kwa sasa inahudumia zaidi Manispaa ya Kinondoni. Hospitali ya Sinza Palestina iliyobaki katika Wilaya ya Ubungo haina hadhi na uwezo wa kutoa huduma kwa Manispaa nzima. Hivyo, Wizara ichukue hatua za haraka za kuboresha huduma katika hospitali hiyo ya Palestina ilingane na wajibu wa kutoa huduma kwa Manispaa mpya ya Ubungo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, hospitali hiyo iko mbali na Jimbo la Kibamba lenye Kata za Goba, Saranga, Msigani, Mbezi, Kwembe na Kibamba; na pia kimuundo Wilaya ya Ubungo inapanuka kuelekea Kata hizo za pembezoni makao makuu ya muda ya wilaya yakiwa kwenye Kata ya Kibamba na ya kudumu yakitarajiwa kujengwa kwenye Kata ya Kwembe. Kadhalika kuna ujenzi wa Mji Mpya wa Viungani (Satelite town) katika eneo la Luguruni hivyo, ni muhimu kukawa na mkakati wa kupandishwa hadhi kituo cha afya kuwa hospitali ya wilaya na zahanati kuwa, kituo cha afya katika kila mojawapo ya kata hizo za pembezoni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, natambua kwamba, kuna hospitali kubwa katika Chuo Kikuu cha Afya (MUHAS), Campus ya Mloganzila. Hata hivyo, hospitali hii hadhi yake itakuwa sawa na Hospitali ya Taifa ya Muhimbili hivyo, haitakuwa rahisi kwa wananchi wa Jimbo la Kibamba kupata huduma za kawaida zinazotolewa na vituo vya afya na hospitali za wilaya. Hivyo, ni vyema Wizara ikafanyia kazi mchango huu na kunipatia majibu yanayostahili.