Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

Hon. Edwin Mgante Sannda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.

MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa fursa, kwanza kabisa niipongeze Waziri, Wizara na timu yake nzima kwa uwasilishaji mzuri. Napenda kusema machache kwa maana ya kuboresha na kurekebisha pale ambapo panahitaji marekebisho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nataka niongelee kuhusiana na hospitali yetu ya Kondoa ambayo kabla ya kugawanywa Halmashauri kidogo tulikuwa tunakwenda vizuri, lakini sasa hivi kutokana na utaratibu bajeti yake imebaki kuwa kutokana na idadi ya watu wanaotokana na Halmashauri ya Mji Kondoa ni kidogo sana. Inapigiwa bajeti kwa ajili ya watu 68,000 wakati inahudumia watu 250,000 wa Kondoa Vijijini, inahudumia watu wa Chemba karibu 250,000, kwa hiyo jumla inahudumia watu karibu 600,000 ingawa inatengewa bajeti kwa ajili ya watu 68,000. Kwa hiyo uwezekano wa kutoa huduma kwa ufanisi haupo kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri nakuomba sana jambo hili pamoja na kwamba tunaangalia kigezo cha population, hebu tuende mbele zaidi, hospitali hii inahudumia na akina nani wengine?

Mheshimiwa Mwenyekiti, babaraba ya kutoka Dodoma - Kondoa kwenda Babati inaeelekea mwisho kumalizika kwa kiwango cha lami. Sasa hivi tena ndiyo tatizo linaongezeka kutakuwa na wasafiri pale watakaohitaji huduma, wako hata jirani zetu wa Wilaya zingine za pembezoni nao wanapata huduma pale. Ninakuomba suala hili la kuangalia kigezo hiki cha idadi ya watu peke yake kwa hospitali kama ya Kondoa najua na wengine wapo wanakumbana na matatizo kama haya, hebu tuliangalie tuweze kutoa huduma hii vizuri kuliko ilivyo sasa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikiwa hapo hapo niongelee kidogo kuhusiana na upungufu wa Miundombinu na vifaa muhimu. Kwanza kabisa ni ambulance, pongezi kwa kazi ambayo tayari imeshafanywa kwa Halmashauri nyingine kupata ambulance, ninakuomba Shemeji yangu Mheshimiwa Waziri Dada Ummy kwamba itakapofika awamu ya pili basi na mimi niwepo katika Halmashauri ambazo zitafuata awamu ya pili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tunachangamoto kubwa sana ya mortuary, mortuary ina uwezo wa kuchukua miili minne tu, kwa hospitali kubwa namna ile miili minne ni kitu kidogo sana. Tunahitaji kufanya utaratibu kuongeza facility hii. Hata maabara nayo ni changamoto. Upande wa madaktari pia tuna upungufu, ninakuomba katika utaratibu wako basi na kwenyewe utufanyie mpango.

Pia niongelee suala la dawa, tunazungumza hapa bajeti ipo vizuri fedha zimepelekwa, lakini Mheshimiwa Waziri hoja isiishie tu kwenye fedha zimepelekwa. Fedha zipo lakini ukitafuta mrejesho kwa wananchi huku dawa hazipatikani. Wananchi siyo kwamba wanaangalia fedha zimeingia au wanataka maelezo, wanataka dawa ziwepo, kuna tatizo pale. Kuna tatizo ambalo nahisi kwenye utaratibu wa manunuzi lakini pia na madaktari wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kushauri vitu viwili, namba moja tupate wataalamu ma-expert wa manunuzi ili supply chain ya madawa iweze kwenda vizuri isije ikafika wakati dawa zinakatika hela ziko kwenye hospitali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili labda tutengeneze muundo wa ki-digital ambapo madaktari watakuwa wanajua stock gani ipo ndani kiasi kwamba hata anapo- prescribe dawa zile anajua dawa zilizopo, siyo daktari anatoa dawa kumbe kwenye stock hakuna. Sasa tutengeneze mfumo ambapo kila zinapotumika, zinapopungua anajua kiasi cha dawa zilizopo na ni dawa za aina gani. Hiyo itatusaidia sana kupunguza hii changamoto.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kule site watu hawaangalii hela, wanaangalia dawa zipatikane. Ninaomba sana Mheshimiwa Waziri jambo hili na mtuambie tu sasa hivi kuna mechanism gani ya kwenu kuhakikisha kweli dawa zinafika na mnapata mrejesho na mfumo gani unawekwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu nataka kuzungumza kidogo kuhusiana na…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa Sannda.