Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Waziri na Naibu wake pamoja na uongozi mzima wa Wizara hii kwa jitihada na kazi kubwa wanayofanya katika kusimamia majukumu makubwa ya Wizara hii. Wizara hii inasimamia majukumu ya rasilimali muhimu ya nchi yetu kwa maana mbuga zetu za wanyama, misitu yetu ya asili pamoja na vivutio vya nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara hii inachangia kwa kiasi kikubwa Pato letu la Taifa kutokana na ujio wa utalii, mazao mbalimbali ya asili mfano magogo ya mbao, lakini bado jitihada za dhati zinahitajika ili kusimamia maeneo haya pamoja na kuongeza usimamizi wa uvunaji wa misitu yetu, Serikali inapoteza fedha nyingi kutokana na watu wengi wasio waaminifu wanaoshirikiana na Watanzania wasio wazalendo kuhujumu misitu yetu. Lazima Wizara ihakikishe udhibiti mkubwa unafanyika. Mfano katika Jimbo langu la Kilindi, Kata ya Msanja, Kitongoji cha Twile kuna uharamia mkubwa wa ukataji wa miti na magogo hivi hawa Wakala wa Misitu (TFS) wanafanya kazi gani? Mimi nadhani kama hawashirikiani na wahalifu hawa basi hawajui makujumu yao, mara nyingi wanapokamata magogo haya yanapelekwa Handeni badala ya kusafirishwa Kilindi, huu ni utaratibu gani? Nashauri Wakala hawa pia ofisi zao zihamishwe au zianzishwe ama kufunguliwa Wilayani Kilindi, eneo hili la uharibifu wa misitu halina usimamizi wa dhati. Nashauri Wizara husika iangalie namna ya kuwa na njia sahihi ya kuwasimamia watumishi wasio waaminifu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa pia kuchangia namna ambavyo Wizara inaweze kupanua maeneo ya utalii kwa kuongeza maeneo ya utalii. Mfano, katika Jimbo langu la Kilindi yapo maeneo mengi ya utalii ambayo tanaweza kuchangia pato la Wizara hii, mfano pori tengefu la Handeni milima ya asili ya Kimbe, milima ya Kilindi asilia, milima ya Lulago yenye miti na uoto wa asilia haya yote ni maeneo muhimu sana ambayo wataalam wake tuijenge nchi. Nashauri ijenge utaratibu wa kufuatilia haya tunapowaambia kwani yana lengo la kuchangia pato la nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ambalo ningependa kuchangia ni upungufu wa wafanyakazi katika Wizara hii ambao wangekuwa na jukumu la kusimamia na kuelimisha jamii juu ya umuhimu wa misitu na rasilimali ya nchi yetu, mfano katika Jimbo na Wilaya yangu ya Kilindi hatuna Afisa wa Wilaya anasimamia misitu, aliyepo ni Afisa katika ngazi ya Kata, Wizara ituletee mtumishi haraka kwani maeneo mengi katika Wilaya yanaharibiwa kwa kukosa usimamizi wa dhati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni juu ya maeneo ya hifadhi za misitu yaliyopo karibu kabisa na mijini, hifadhi hizi pamoja na faida tunayopata ya kuhifadhi mazingira na kupata mvua lakini maeneo haya yamekuwa ni maficho ya wahalifu hasa majambazi. Mfano msitu wa pale Kipala mpakani Wilaya ya Mkuranga hifadhi hii majambazi yametumia kama mafichio na hata askari zaidi ya sita wameuwawa pale kwenye check point. Nashauri Wizara sasa isafishe kwa kukata miti kwa mita 50 ili kuleta ulinzi na usalama kwa wakazi wa eneo hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema haya naunga mkono hoja.