Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Eng. Joel Makanyaga Mwaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chilonwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. JOEL M. MAKANYAGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi nami niweze kuchangia katika Wizara hii ya Ardhi. Kwanza kabisa nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia uhai sisi sote tuliomo humu ndani, tumekutana leo tuweze kuifanya kazi hii muhimu kwa Watanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niendelee kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuendelea kututunzia Rais wetu Mheshimiwa Rais. Dkt. John Pombe Magufuli tukitambua na kazi yake kubwa aliyonayo. Tunaomba aendelee kumtunza aifanye kazi kwa uaminifu kadri atakavyomjalia. Mwisho, nimpongeze Mheshimiwa Waziri wa Wizara ya Ardhi, kwa kuleta hotuba nzuri hapa, ambayo tumeisikia ina mantiki na changamoto nyingi ambazo tunazijadili sasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, labda nianze tu kwa kusema kwamba, nionavyo mimi ardhi ni eneo muhimu sana katika safari yetu hii tuliyoianza ya kuelekea kwenye Tanzania ya uchumi wa kati. Kama tulivyokwishaona katika mijadala yetu mbalimbali tuliyofanya ya Wizara ambazo tungezifanya kama viwanda, kilimo na mifugo, ujenzi na kadhalika. Wizara zote hizi tumezijadii zikizingatia mpango wa maendeleo wa miaka mitano ambayo ndani yake sasa tunajadili mpango wa maendeleo wa mwaka mmoja mwaka 2016/2017.
Mheshimiwa Mwenyekiti, labda nianze sasa kwa kumpongeza kwa dhati Mheshimiwa Waziri kwa hotuba yake nzuri iliyoenea na kusheheni kila kile tunachokitegemea Watanzania nini kipo, nini tunakitegemea. Hata hivyo, niseme kwamba, nitoe mfano ambao tunaujua wote kwamba, nini kilianza kuku au yai, kila mtu ana majibu yake humu ndani, lakini nikikuuliza Wizara ipi muhimu katika Wizara zetu nyingi tulizonazo kila mtu atakuwa na majibu yake vilevile lakini nitakwambia Wizara ya Ardhi iko mbele. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, iko mbele na wachangiaji wote waliopita wamekwisha yasema haya, Wizara ya Viwanda haitakuwepo kama hakuna ardhi utavijenga wapi hivyo viwanda, Wizara ya Kilimo na Mifugo utalima wapi, utafuga wapi kama ardhi haipo, ujenzi yawe wa barabara au nini utatengeneza wapi barabara kama hakuna ardhi, lakini kikubwa ni wapi unalima, wapi unajenga na wapi unafuga.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ndio kazi kubwa ambayo Wizara ya Ardhi inayo na ndiyo haya ambayo Mheshimiwa Waziri amejitahidi sana kuelezea mikakati na mipango aliyonayo angalau kwa mwaka huu wa 2016/2017, nini wanatarajia kama Wizara kukifanya. Niseme kama kuna tatizo kubwa katika Wizara hii ni migogoro ya ardhi, imekithiri na imedumu muda mrefu shida ni nini? Shida iko wapi? Kwa nini hatuitatui, kwa nini haifiki mwisho? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kupitia kwako nichukue mfano wa kwangu Wilaya ya Chamwino na hasa Jimbo la kwangu la Chilonwa, Mheshimiwa Waziri Lukuvi, alishawahi kuwa Mkuu wa Mkoa hapa Dodoma, analifahamu sana Jimbo langu la Chilonwa, anafahamu sana matatizo ya ardhi yaliyopo Jimbo la Chilonwa, maeneo ya Kata ya Segala kule Izava, kule Walii ambako tumepakana na Wilaya ya Kongwa anafahamu sana tatizo la migogoro lililopo kule Dabalo katika Vijiji vya Chiwondo ambavyo pia vimepakana na Kongwa, kule hakuna usalama. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi sasa, wafugaji wanaleta fujo sana. Ninavyozungumza hapa nilipo wanaingiza mifugo kwenye mashamba ya wakulima, huku wakiwa wamejiandaa na mikuki na mishale, mkulima atokee wampige mishale, hakuna amani. Nimuulize tu Mheshimiwa Waziri, kuna mpango gani wa kutatua haya matatizo ambayo yameshakuwa ya muda mrefu, shida ni nini? Ukiangalia maeneo niliyoyataja maeneo ya Izava, Walii na Chiwondo yanapata huduma zote za kijamii toka Wilaya ya Chamwino, kuanzia maji, shule, ikija wakati wa sensa, kujiandikisha kupiga kura, hata mimi mwenyewe nimepigiwa kura na hawa, lakini ikifika wakati wa kilimo tayari utaona migogoro imeanza wanakuja wafugaji wanaotoka maeneo ya Kongwa wakidai kwamba yale maeneo ni ya Kongwa. Inaonekana labda kweli ni maeneo ya Kongwa, Serikali iko wapi wakati siyo wa kilimo kuingilia na kutatua yale matatizo once and for all. Shida ni nini? Kwa kweli niseme tu, sitaki kuingia kwenye historia lakini niseme kama hakutakuwa na maelezo mazuri wakati Mheshimiwa Waziri una-wind up…
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja.