Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Julius Kalanga Laizer

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Monduli

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na umuhimu wa Wizara hii ya Nishati na Madini na kutokana na changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika Wizara hii hasa katika Mkoa wa Rukwa, napenda kuchangia mambo yafuatayo:-
Suala la TANESCO kuwadai wananchi pesa za nguzo. Suala hili limekuwa likileta shida kwa wananchi wetu hasa pale wanapohitaji huduma hii muhimu ya nishati katika Mkoa wa Rukwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, elimu kwa watu walio karibu na nguzo. Suala hili limekuwa na changamoto nyingi, hasa katika Mkoa wangu wa Rukwa. Naishauri Serikali kutoa elimu kwa wananchi wetu wajue athari zinazoweza kujitokeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kukatika kwa umeme bila taarifa. Suala la kukatika kwa umeme katika Manispaa ya Sumbawanga limekuwa likiwaathiri sana wafanyabiashara, hasa pale wanapokosa taarifa ya kukatika kwa umeme na kuleta athari kubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la maeneo mengi kukosa umeme. Katika Mkoa wa Rukwa na Wilaya zake kuna shida kubwa ya kukosa umeme mpaka leo. Je, Serikali au Wizara ina mkakati gani wa haraka wa kupeleka umeme katika Wilaya ya Nkasi, Wilaya ya Kalambo na Sumbawanga Vijijini?
Mheshimiwa Naibu Spika, ni vigezo gani vinatumika katika kufikisha umeme vijijini, REA III? Kutokana na kutambua kuwa Mkoa wa Rukwa uko Tanzania, lakini ni maeneo mengi katika mkoa huu wananchi wengi hawajafikiwa wala kuwa na dalili zozote za kupelekewa umeme!
Mheshimiwa Naibu Spika, gharama halisi za mtu kuvuta umeme. Kumekuwa na hali ya manung‟uniko kwa wananchi wanapokuwa wanahitaji kuingiza umeme katika nyumba zao, wamekuwa wakiambiwa bei tofauti tofauti. Je, ni kiasi gani wananchi wanapaswa kutoa?
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kukatika kwa umeme mara kwa mara katika Manispaa za Sumbawanga na Nkasi. Hali hii imekuwa ikijitokeza mara kwa mara, je, Wizara inatambua suala hilo na je, kuna utaratibu wowote wa kumaliza tatizo hilo?
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la madini yanayopatikana Sumbawanga. Napenda kujua kama Wizara inajua kuwa kuna madini yanapatikana Manispaa ya Sumbawanga? Kama ndivyo, wameweka mkakati gani? Kwani mpaka sasa mambo yanayofanyika ni kinyume kabisa na umiliki wa vitalu na madini yetu yanakwisha.