Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Naibu Spika, shukurani kwa Waziri, Naibu Waziri na wataalam wa Wizara kwa hotuba nzuri yenye kuleta matuamini kwa Watanzania. Mradi wa umeme wa REA kwa Kisiwa cha Mafia umebakiza vijiji na maeneo 10 kukamilika, navyo ni vijiji vya Gonge, Jojo, Mariam, Bani, Jibondu, Juani, Chole, Dongo na Maeneo ya Tumbuju, Bwejuu na Tongani. Ombi langu kwa Wizara ni vijiji na maeneo husika viingizwe kwenye mradi wa REA Phase III.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ni uzalishaji wa umeme kwa sababu umeme Mafia unatokana na chanzo cha mafuta yanayoendesha majenereta yaliyopo. Kutokana na gharama kubwa ya ununuzi wa mafuta na matatizo ya usafiri wa mafuta hayo kwa njia ya bahari, ombi letu wananchi wa Mafia ni kwamba, Serikali sasa iunganishe na umeme wa SONGAS kupitia kupitishwa kwa submarine cable kutokea Nyamisati kwenda Kilindini takriban kilomita 50 ili kuondokana na adha ya kusafirisha mafuta mara kwa mara.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la utafiti wa mafuta na gesi, katika Kisiwa cha Mafia ni jambo linalofanywa mara kwa mara. Kwa habati mbaya sana wananchi wa Mafia wamekuwa hawapewi taarifa tunaomba Wizara na Waziri wakati atakapokuwa anajibu awaeleze wananchi wa Mafia kama mafuta au gesi vimegundulika Mafia au hapana ili kuondoa hali ya sintofahamu kwa wananchi wa Mafia.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine kwenye ugunduzi wa gesi hasa maeneo ya kina kirefu cha bahari yaani off share maeneo ya Kusini mwa Tanzania. Mpakani mwa Wilaya ya Kilwa na Mafia, katikati ya bahari kuna visima viwili ambavyo kimpaka kimo katika Wilaya ya Mafia, lakini kutokana na matatizo ya usafiri shughuli za uchimbaji na utafiti zimekuwa zikifanyika kutokea Wilaya ya Kilwa.
Swali je, wananchi wa Mafia wananufaika vipi na visima hivi ambavyo kimipaka vipo Mafia lakini shughuli za uchimbaji zinafanyika Kilwa?
Suala lingine ni bomba jipya la gesi kutoka Kusini kuja Dar es Salaam, ujenzi umekamilika kwa asilimia 100. Swali, je, ni lini bomba litaanza kusafirisha gesi kutoka Kusini kwa matumizi ya kibiashara? Swali lingine, ni lini umeme ghafi utachakatwa na kuweza kutumika kwa matumizi ya majumbani?
Mheshimiwa Naibu Spika, natanguliza shukurani na naunga mkono hoja.