Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025 na Mapendekezo ya Mwongozo wa Maandalizi ya Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025

Hon. Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025 na Mapendekezo ya Mwongozo wa Maandalizi ya Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi. Kwa sababu ya muda niruhusu nimpongeze Rais peke yake. Tunampongeza Rais kwa kuleta mapendekezo ya Mpango huu na mpango huu kwa mara ya kwanza unakuja wakati tuna Tume mpya ya Mipango na sheria mpya na Wizara maalumu inayoshughulikia mipango ya Serikali. Kwa hiyo, tunampongeza Mheshimiwa Rais kwa ukweli kwa direction hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile nampongeza Rais kwa hatua ambazo zina maana kubwa sana, maridhiano, ustahimilivu, mageuzi na kujenga upya. Nilivyokuwa nasoma Hotuba ya Profesa Kitila Mkumbo, kwanza is very radical, hotuba Fulani, imechukua angle fulani hivi ambayo ndiyo tunataka. Tunataka mipango ambayo inaelekezwa kwenye vijiji vyetu. Watanzania walio wengi wako vijijini, hivyo, tunataka focus ya mpango huu iende kweney rural development. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia data za Serikali hapa, mikopo ya biashara shilingi trilioni 22 halafu second percent peke yake ndiyo imeelekezwa kwenye kilimo, wafugaji na wavuvi. Hii haiwezekani, hapana. Kama ni kweli tunataka twende kwenye rural development, lazima tuweke pesa nyingi sana kuelekeza kwenye kilimo, mifugo na uvuvi. Kwa sababu, ndiyo Watanzania wengi wako huko. Tukiwa na mipango ambayo ina-move na watu walio wengi, hapo ndiyo tunazungumzia habari ya maendeleo. Maendeleo ni watu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, haiwezekani kila wakati tunakuja hapa halafu tunasema tunawekeza kwenye kilimo, kwenye ufugaji na uvuvi lakini hatuoni, haiwezekani. Kwa hiyo, Mheshimiwa Profesa Kitila assignment yako ya kwanza sasa, tunataka hii rural economic development tuione, huko vijijini siyo kwenye vitabu. Tunataka tutoke kwenye vitabu sasa. Hii nchi ina documents nyingi, nzuri sana, lakini tukienda kule kwenye vijiji vyetu hatuoni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati naangalia hii, ni kweli wafugaji wametajwa, wakulima wametajwa na wavuvi, lakini ukisoma hii huoni tangible, vitu ambavyo vinamhusu mtu anaitwa mfugaji. Waziri amezungumzia habari ya kuwa na viwanda na kuziongezea thamani products zinazotokana na mifugo. Honestly hivi ipi ya kwanza, ni mahali pa kuhifadhia hii mifugo au wanataka viwanda? I think Ilani yetu ya Chama Cha Mapinduzi ukurasa wa 52 tuliweka commitment kwamba, kuhakikisha tunatenga maeneo ya ufugaji yapimwe na infact tumeweka mpaka statistics, mpaka zifike hekta milioni sita. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani kabla hatujazungumza habari ya viwanda, lazima tuwe na maeneo ambayo yamelindwa kisheria. Tukishakuwa na maeneo hayo ndiyo tuzungumze habari ya viwanda. Kwa hiyo, tunataka bajeti zijazo na Mpango wake tuone bajeti kubwa ikienda kwenye maeneo haya. We are not interested in reading nice documents, tunataka kuona tangible results. Nilikuwa nasoma hapa mpango wetu huko kwa wakulima; “kuendeleza juhudi za kujitosheleza kwa mahitaji ya chakula nchini na kuendelea kuongeza matumizi ya mbolea, mbegu bora na kilimo na umwagiliaji”. That’s fine, lakini trekta ziko wapi hapa? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Serikali inataka wakulima hawa na wakulima wa nchi hii wanafanya kazi kubwa sana, pamoja na kwamba wakati mwingine wanapata statements za ajabu ajabu. Wanaambiwa wanalima kienyeji, wanafuga kienyeji, lakini hizi hizi documents ndizo zinazosema the reason we have fought self-sufficient zaidi ya asilimia 120, ni kwa sababu ya wakulima hawa. Wanalima hivyo hivyo mnavyoita kienyeji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mbona hapa tunaona hifadhi ziko nyingi sana, karibu sijui ishirini na ngapi na mapori tengefu. Ukiangalia size ya hiyo, lakini uki-compare na nchi kama Namibia, ina National Parks saba tu. Halafu ukiangalia tunapata nini kutokana na mapori haya au na sisi tuseme mnahifadhi kienyeji kienyeji hivi? I think it is high time twende kwenye quality. Alizungumza Mheshimiwa Mbunge wa Mbarali jana hapa, “Development must be people centered. There is no question of development where by human beings in individuality is being destroyed for the sake of wildlife,” haiwezekani! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lazima watu kwanza. Hata hili lililotokea hapa leo tusipoweka emphasis kwenye kutetea watu, maendeleo hayana maana. Lazima, a true definion ya maendeleo must start from a human perspective. Mheshimiwa Profesa Kitila, hapa tunazungumzia habari ya utawala wa sheria, kama nguzo ya maendeleo yetu kama Taifa, nakubaliana, as a lawyer I agree. But what is the rule of law kama sheria zetu na hapa naongelea msingi huo wa reforms. Mheshimiwa Rais anataka reforms, lakini tuna sheria za kikoloni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, eti mfugaji ng’ombe wameingia shambani halafu we are not interested with a fine, eti una-forfeit. Una wa-impoverish watu halafu tunazungumza habari ya mipango, wakati sisi na mpango huu tulitaka Watanzania watajirike. Sasa, lazima tuamua, tuendelee kuwa na sheria ambazo zinawa-impoverish watu ama tuwe na sheria ambazo nia yake ni kukataza matatizo yasitokee. Unapo-forfeit ng’ombe leo unam-impoverish huyo mtu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii inatokea kwa sababu ya kuwa na sheria tu ya kikoloni. Mheshimiwa Attorney General, sijui kama yuko hapa. Hii forfeiture, hii section ipo, tangu Sheria ya mwaka 1958 na tumepata uhuru. We cannot question … (Makofi)

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Edward Olelekaita kuna taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Ester Bulaya.

TAARIFA

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampa taarifa kaka yangu Mwanasheria kwa mchango mzuri sana kuhusiana na masuala ya utekelezaji wa sheria. Hivi tunavyoongea Jimbo la Bunda Mjini, Kata ya Kunzugu, familia 16, ng’ombe 500 wameshikiliwa na TANAPA na wana mpango wa kuwataifisha, lakini Mahakama imetoa ruling walipe faini. Wananchi wanataka kulipa faini ili waokoe ng’ombe wao, lakini TANAPA wanakataa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nampa hiyo taarifa. (Makofi)

MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Olelekaita, unaipokea taarifa?

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipokea sana.

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, …

MWENYEKITI: Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii.

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii. Naomba Mheshimiwa Bulaya atupe uthibitisho wa hiyo hukumu inaelekeza nini ili na sisi tuweze kuthibitisha kwa upande wa TANAPA na kuweza kuchukua hatua kama ni kweli Mahakama imeruhusu waweze kulipa faini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha. (Makofi)

MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Edward Olelekaita, malizia mchango wako.

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Sasa, sijui hata nisemeje. Siji nipokee ile ama nifanye nini, anyhow. Niseme hivi, in fact kama Mheshimiwa Waziri, anataka tulete hizo kesi ziko nyingi sana, lakini iko hivi, kwa sababu lazima sasa twende a step further. Tukileta atafanya nini? (Makofi)

MHE. RIZIKI S. LULIDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nilindie muda wangu.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Mbunge, kuna taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Lulida.

TAARIFA

MHE. RIZIKI S. LULIDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nakushukuru kunipa hii nafasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna sheria na kuna mipaka ilishatengenezwa, corridor za wanyamapori na binadamu, lakini vile vile hao wafugaji. Leo wako katika Mkoa wa Lindi. Vurugu za wafugaji kuvamia maeneo na mashamba ya wananchi zimekuwa kubwa, mpaka wananchi wameuawa na wafugaji. Tusiendelee kukubali vitu ambavyo havitaki kufuata sheria. [Maneno Haya Siyo Sehemu ya Taarifa Rasmi za Bunge]

Mheshimiwa Mwenyekiti, twende na sheria, Serikali ina sheria yake na wafugaji watii sheria ya nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kumpa taarifa hiyo. Sasa hivi twendeni Lindi mkaone migogoro ya wafugaji kuvamia maeneo ya wakulima na kuleta kero kubwa katika mazingira haya, ahsante sana.

MWENYEKITI: Ahsante sana.

MHE. CHRISTOPHER O. OLE-SENDEKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mwongozo wa Spika.

MWENYEKITI: Ngoja, Mheshimiwa Riziki, tunashukuru kwa taarifa yako. Hii taarifa ulikuwa hunipi mimi, ulikuwa unampa Mbunge anayechangia. Mheshimiwa Olelekaita, endelea na mchango.

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na namheshimu sana mama yangu Mheshimiwa Lulida. Nilikuwa naongelea kitu tofauti kidogo. Nilikuwa nasema hivi, hapa tunaongea na Waziri wa Mipango ya Nchi hii by the way. Kwa hiyo, wengine watulie kidogo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunachosema hapa mipango ya nchi na Mheshimiwa Profesa Kitila amesema vizuri sana hapa, amezungumza jambo sawa. Amesema, Mpango wa Maendeleo wa Taifa siyo mpango wa Serikali and it is true. Tutatarajia sasa kabla ya ule mpango mkubwa kuja, sasa waje watwambie wamewa-consult watu akina nani. Pengine this time, hebu waanzishe mjadala wa Kitaifa tuzungumze habari ya Mpango huu wa Taifa, kwa sababu nakubali, siyo mpango wa Serikali, ni mpango wa Taifa letu. Kwa hiyo, hiyo statement ni nzuri sana, tunataka tuone. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa wameongelea kuhusu watumishi wa umma na ni kweli, engine ya mipango ya yote ya Serikali ni watumishi wa umma and I agree with you, amem-quote mpaka Waziri Mkuu wa Singapore. Kama tunataka kufuata njia ya Singapore unajua lazima tuwe na discipline sasa. It is not enough kusema twende kama Singapore, no! Lazima tujue Singapore wamefanya nini ili tutembee kwenye hiyo barabara. Hapa Waziri ametengeneza quotation nzuri sana na watu wengine huwa wanafikiri, kuna wakati Singapore pia walianza kufikiri mfumo wa elimu yao pengine sio mzuri kama tulivyo leo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, watu wengine wanasema hivi, unajua kwa nini Marekani watu wao ni innovators na ukiangalia wale watu wakubwa, sio kwamba walikuwa na distinctions kwenye universities, no! tofauti ya vyuo vyetu na nchi nyingine, kwa mfano kama Marekani, wao wanachoangalia they are interested in who you are as person rather than the test ulizopata kwenye distinction yako. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, they appreciate those who take bold decisions, those who do nothing, do things differently, those who overcome problems, those who are street smart, those who see the world for what they can do, not what they cannot do. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukiwa na sheria ambazo zinaleta barriers leo, badala ya ku-support hizo innovation na watu wa umma, sisi tumeletewa Ripoti ya CAG hapa. That is a very good test, kama tunataka nidhamu kwa sababu Waziri amesema ndio nguzo ya mpango huu, ni kutekeleza ripoti kama za CAG, lakini tutakwenda a step further na kusema what is wrong with recruitment? Halafu tubadilishe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na naunga mkono hoja. (Makofi)