Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2021 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023

Hon. Kavejuru Eliadory Felix

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2021 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023

MHE. KAVEJURU E. FELIX: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa fursa hii nami nichangie kwenye hotuba ya Waziri wa Fedha na Mipango kwa mwaka 2022/2023. Kwanza nianze kwa kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuijenga nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue nafasi ya pekee kuwapongeza Waziri wa Wizara ya Fedha, Naibu wake na Watendaji wote wa Wizara ya Fedha kwa kutuletea bajeti ambayo kabisa inaonesha nia ya dhati ya kujenga uchumi shindani na viwanda kwa maendeleo ya watu. Hongereni sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mchango wangu unaenda kujikita kwenye uchumi wa bluu kama sehemu mojawapo ambapo bajeti hii imeweka kipaumbele katika sekta za uzalishaji. Uchumi wa bluu unamaanisha mazao, uchumi unaotokana na uvunaji kutoka kwenye maji ya bahari, maziwa, mito, mabwawa na kadhalika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Sekta ya Uvuvi inakua kwa asilimia 2.5 na inachangia pato la Taifa kwa asilimia 1.8 na inaajiri zaidi ya Watanzania milioni 4.5. Kiwango cha pato kinachochangiwa na sekta hii muhimu ambayo Mwenyezi Mungu ametujalia kuwa na maziwa makubwa katika Bara la Afrika ambayo yanapatikana Tanzania ambayo ni Victoria, Tanganyika, Rukwa, Nyasa na ukanda mkubwa wa bahari na maziwa mengine madogomadogo ambayo ni Eyasi, Natron, Manyara. Kwa maliasili yote hiyo ambayo Mwenyezi Mungu ametupa na ukalinganisha na mchango unaochangiwa na maliasili hii ni mdogo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijikite kwenye Ziwa Tanganyika. Ziwa Tanganyika kabla ya uhuru ndiyo ziwa ambalo lililokuwa likichangia pato kubwa kwenye uchumi wa mkoloni. Tunapozungumza Ziwa Tanganyika, tulichozawadia dhahabu ya kwanza ya Ziwa Tanganyika ni dagaa, kwa jina maarufu dagaa wa Kigoma. Zawadi nyingine ya pili inayopatikana katika Ziwa Tanganyika ambayo tulipewa inaitwa ni almasi ambayo ni migebuka. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Ziwa Tanganyika lina aina za samaki zaidi ya 224 lakini samaki ambao ni wa kibiashara (commercial fish species) ziko mbili tu na sana ukiongeza ya tatu ni moja. Ya kwanza ni dagaa, ya pili ni migebuka na ya tatu ni sangara. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2000 ziwa hili limedoroka katika mapato yake. Wavuvi wamekuwa wakihangaika, hawana miundombinu, lakini kitu kikubwa zaidi tunachoweza kukiangalia ni kipi. Naomba niende kwenye chimbuko lenyewe la uzalishaji la mapato ya Ziwa Tanganyika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, katika miaka ya 1990 hadi 2000, uvuvi katika Ziwa Tanganyika, wastani wa mapato ilikuwa ni metric tons 200,000 na mwaka 2000 hadi 2013 uvuvi ulishuka hadi tukawa tunavuna kwa wastani wa metric tons 120. Kwa 2013 mpaka sasa inasemekana kiwango tunachokipata ni metric tons 80. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kushuka kwa mapato ya uvuvi yanatufikirisha sana. mwaka 1953 wakati wa utawala wa wakoloni, Mwingereza alipoona Ziwa la Victoria halina mapato makubwa yeye alichukua sangara kutoka katika Ziwa Tanganyika na kupeleka Kamati ya Utafiti ya Uvuvi ya Kikoloni ilichukua sangara kutoka katika Ziwa Tanganyika na kuipeleka kupanda katika Ziwa Victoria. Uchumi tunaoshangilia sasa hivi wa sangara umetokana na kazi nzuri iliyofanywa na mkoloni. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tujiulize, tafiti zetu za uvuvi (TAFIRI) je, hawana mpango au wana upungufu wa fedha hawawezi wakafanya utafiti kuangalia namna gani ambavyo wanaweza wakachukua sangara wakaweka kwenye maziwa haya mengine ambayo siyo productive kama Ziwa Rukwa na Eyasi? Nashauri sana Idara ya Utafiri ya Uvuvi (TAFIRI) waongezewe fedha ili waweze kufanya utafiti. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu kushuka kwa mapato katika Ziwa Tanganyika, sasa hivi kuna zoezi linaloendeshwa na Serikali yetu ya fish stock assessment ambayo inafanyika upande wa Tanzania. Samaki walioko katika Ziwa Tanganyika ni pelagic ni migrant wana-move. Ili zoezi hili liwe na tija, basi ni vema nchi yetu ishirikiane na nchi zile ambazo zote zina-share Ziwa Tanganyika ambazo ni Burundi, Congo na Zambia. Hilo zoezi lifanyike kwa pamoja, zoezi hilo litaleta tija. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nihamie kwenye nishati kwa maana ya kuleta msisimko wa kuleta viwanda nchini Tanzania. Nimepita nikiangalia nchi zilizoendelea, nchi zilizoendelea nyingi zilifanya utafiti na kuhakikisha kwamba zina nishati ya kutosha. Kwa mfano, Afrika Kusini ina megawati 80,000, Uturuki ina megawati 60,000. Sisi tukiangalia vyanzo vyetu pamoja na umeme uliopo vyote kama tutakuwa tumeviendeleza, tutaweza kupata megawati 5,579.8. Umeme ndiyo moyo wa viwanda…(Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Ahsante Mheshimiwa Felix kwa mchango mzuri na hongereni kwa dagaa wazuri.

MHE. KAVEJURU E. FELIX: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.