Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2021 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023

Hon. Tecla Mohamedi Ungele

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2021 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023

MHE. TECLA M. UNGELE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya mimi kuchangia bajeti kuu. Awali ya yote ninampongeza Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuweka kipaumbele kuridhia mradi wa LNG kule Lindi kwa hiyo sisi wana Lindi na Mtwara na Taifa kwa ujumla tunashukuru. Hili ninajua kabisa ni kwa ajili ya ustawi wa Taifa letu. Ninampongeza pia Waziri wa Fedha na Mipango Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Nchemba na timu yake yote kwa kuja na bajeti kuu hii nzuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mchango wangu nitajikita kwenye Mkakati wa Taifa wa Kupambana na Kukabiliana na Ukatili katika Jamii. Nakuja na takwimu chache tu angalau, Mpango Mkakati wa Kutokomeza Ukatili kwa Wanawake na Watoto (MTAKUWA) mwaka 2017/2018 hadi 2021/2022 ulidhamiria kupunguza ukatili katika jamii yetu kwa asilimia 50. Ukatili huu ni wa kimwili, kisaikolojia, kingono na hata kiuchumi. Pia kuna taarifa, walifanya hawa MTAKUWA, kwamba kati ya wanawake watano basi mmoja ame-experience ukatili wa kingono. Lakini pia kati ya wasichana watatu mmoja amepitia ukatili wa kingono. Kati ya wavulana saba mmoja amepitia ukatili wa kingono katika maisha yake. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia tafiti za Serikali na UNICEF zimetoa taarifa kwamba ukatili huu kwa asilimia 60 unatokea nyumbani na kwa asilimia 40 unatokea shuleni. Hii ni hatari sana. Mtoto huyu atapona namna gani? Kama akinusurika ukatili pale nyumbani basi akienda shuleni atapata ukatili wa kingono na aina nyingine. Hili ni janga kubwa, tusilifumbie macho, hali siyo shwari. Madhara yake ni nini kwa ukatili huu; vijana wetu na wanawake wanaathirika kimwili, hata viungo vya uzazi vinaathirika lakini kikubwa zaidi afya ya akili inaathirika sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, wanapotendewa tendo hili la ukatili uwe wakingono iwe wa kiuchumi iwe wa kinini basi kijana huyu au mtoto huyu ana weka kumbukumbu zile kwenye sub conscious mind. Kinachotokea jinsi anavyoendelea kukua analeta ile event ama seen, inakuja usoni inakuwa kama screen inaendelea kum-disturb. Kwa maana hiyo sasa nini kinatokea; anakuwa na hofu hana ujasiri ni mwenye mashaka hata akienda shuleni hana mchango mzuri ndio wale unakuta hawana maendeleo mazuri kimasomo. Hii ni hatari sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo katika Serikali yetu sasa, ninaona kwenye bajeti kuu hapa kuna rasilimali zimetengwa Wizara ya Maendeleo ya Jamii imetengewa milioni 43; lakini pia afua maalum za kupambana na ukatili ni bilioni 2.65 kwa Mikoa yote. Ina maana katika Mkoa milioni 14 kwa mwaka. kwa wastani ni milioni moja kwa kila Halmashauri kwa mwezi. Hii ni hatari sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukatili huu ni vita kubwa. Sasa vita kubwa hii tunaenda na silaha kidogo sana. Ninaomba kabisa, bajeti ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii naomba iwe revised na iongezewe. Lakini pia kuna watendaji wetu kule, maafisa maendeleo ya jamii na maafisa ustawi wa jamii, hawa kazi yao kubwa ni kuhamasisha uchumi katika kaya na kuhakikisha kutokomeza mila na desturi potofu zinazosababisha ukatili pamoja na kuimarisha mahusiano katika familia pamoja na. hata hivyo, watu hawa kwanza ni wachache, tumeona katika taarifa, maafisa maendeleo ya jamii wapo asilimia 43 lakini maafisa ustawi wa jamii wako asilimia 97 tu nchi nzima. Sasa vita yoyote…

MHE. NEEMA G. MWANDABILA: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

NAIBU SPIKA: Taarifa

T A A R I F A

MHE. NEEMA G. MWANDABILA: Mheshimiwa Naibu Spika, nilitaka nimpe taarifa mzungumzaji kwamba ustawi wa jamii upungufu ndio asilimia 97, sio kama alivyoongeza ndugu Mbunge. Ahsante sana.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Tecla.

MHE. TECLA M. UNGELE: Mheshimiwa Naibu Spika, afisa maendeleo ya jamii kuna upungufu huo kama nilivyousema na afisa ustawi wa jamii pia upungufu wa asilimia 97.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwakuwa sababu mojawapo ya ukatili katika jamii yetu ni kutokana na changamoto ya uchumi, hivyo basi ile asilimia 10 iliyokuwa imepangwa kwa ajili ya kuhudumia jamii yetu; wanawake asilimia nne vijana asilimia nne, na wenye makundi maalum (walemavu) asilimia mbili ninaomba ibaki vile vile. Hata hivyo tulikuwa tunaomba hata iongezwe ifikie asilimia tisa kwa wanawake. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hii ni hatari sana, kwa sababu hata kwenye halmashauri zetu ile tu iliyokuwa nne nne mbili (4:4:2) haitoshi. Bado kuna mlundikano wa maombi ya jamii yetu kuomba misaada hiyo ama mikopo hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, tafani ninaomba tuiangalie jamii hii, tuangalie kuwakwamua hawa wananchi, hususani wanawake katika jamii yetu. Bila kufanya hivyo ukatili huu utaendelea na matokeo yake huko miaka 50 ijayo miaka 20 ijayo miaka 30 ijayo sijui tutakuwa na Taifa gani la Tanzania lisilojiamini na lisilokuwa na ubunifu kwa sababu tayari wameathirika na ukatili wa kijinsia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuunga mkono hoja. (Makofi)