Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2021 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023

Hon. Prof. Shukrani Elisha Manya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2021 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023

MHE. PROF. SHUKRANI E. MANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi nami ya kuchangia katika Bajeti Kuu ya Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kutambua jitihada za Serikali katika kuongeza bajeti katika sekta za uzalishaji. Jambo ambalo Wabunge wote tumelifurahia, kwamba kuongeza bajeti katika sekta za uzalishaji kwa maana ya kilimo, mifugo na uvuvi, tunakwenda kufanya uzalishaji mkubwa. Na kama tija ambayo tumeiongea sana katika Bunge hili itatokea, basi tunakwenda kujikwamua mahali pakubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nipende kupongeza jitihada na hatua ya Serikali ambayo imetambua kwamba kuna sababu kubwa na ya msingi ya kuziba mianya ya upotevu wa fedha katika matumizi ya Serikali. Jambo la kwanza, Mheshimiwa Waziri wa Fedha alipendekeza juu ya hasara inayopatikana kutokana na watumishi waliopumzishwa majukumu yao. Wabunge wengi wameongelea, na nipende kukumbuka kwamba Mheshimiwa Janejelly alisema kwamba kama Kanuni zetu zinaruhusu basi kweli huo mpango wako uendelee.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini mimi ninapenda kusema kwamba, ili Serikali isipate hasara juu ya watumishi hawa ambao wanapumzishwa majukumu yao, basi muda mchache uwekwe baina ya wao kupumzishwa na kurudishwa katika majukumu yao. Serikali ijipe timeline ni wiki mbili au mwezi mmoja, mtumishi awe amerudi kufanya majukumu yake, lakini anapokaa mwaka mzima, mtumishi huyu kwanza anakuwa demoralized halafu anajisikia ni reject. Sasa Serikali inapata hasara hapa, mtumishi yuko demoralized hapa kwa sababu hajarejeshwa katika kazi yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo hili tufunge loop. Wakati Serikali haitaki kupata hasara tufunge loop upande wa pili mtumishi arudi mapema katika majukumu yake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine katika kupunguza matumizi ya Serikali ni kuhusu matumizi ya magari. Nakupongeza sana Mheshimiwa Waziri juu ya hili; lakini napenda huku nako tufunge loop, kuna loose loops hapa mahali pia. Yaani tumeona hasara inayopatikana kwasababu ya wingi wa magari, lakini Mheshimiwa Waziri wa Fedha wale wakala wa kutengeneza haya magari hebu jiulize unao watumishi wa kutosha kule ndani? Kama hawa watumishi hawatoshi wanaotengeneza wanatoka upande gani? Na kwanini usilipe zaidi ya ambavyo unapaswa kulipa? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo si ajabu ukakuta; nitoe mfano ambao ni rahisi sana; wote hapa tunajua kuwa wind screen ya gari 250,000 lakini inapotoka voucher TEMESA unakuta imekuja mara tatu au mara nne zaidi ya hiyo, wind screen. Huu nimeutoa mfano ambao ni halisi nimekutana nao. Wote tunajua kwamba wind screen ni 250,000 au 300,000 ya Prado au Landcruiser lakini angalia katika voucher zako za matengenezo ya magari yako hutakuta hiyo bei. Mara nyingi utaambiwa 750,000 au 1,000,000. Hapo napo, kwa zile gari ambazo utaamua zibaki kwa wale watendaji wakuu wa Wizara basi hebu funga loop upande wa TEMESA uone kwamba bei unazoletewa za vipuri vya magari ndizo bei halisi za soko kama ambavyo unatamani pia kupunguza upande wa umma procurement. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine; Ofisi ya CAG imependekezwa kuongezewa watumishi na pia kufanya technical pamoja na financial audit. Hata hivyo hiyo bado ni audit. Mimi ninapendekeza, kwasababu kazi yao ni ku-audit na una audit na una audit kazi iliyokwishafanyika sasa tija itatoka wapi? Mimi nadhani kama tuna mpango wa kunusuru nidhamu ya matumizi bora ya fedha za Serikali basi hawa watu katika hii Ofisi ya CAG wapewe pia jukumu la monitoring and evaluation pamoja na kufanya audit. Wakiendelea kufanya audit bado watamkuta mtu ambaye amekwisha kutumia vibaya fedha za Serikali halafu anakuja kuwajibishwa. Sasa, tunapaswa tuzuie matumizi hayo, ambapo ni pamoja na kufanya monitoring and evaluation. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile niongelee kuhusu Wizara ya Maliasili na Utalii, na nitambue mchango mzuri kabisa na maono ya Mheshimiwa Rais ambaye kwakweli amekwenda kutanzua kitendawili ambacho mataifa ya nje; watu wengi wanadhani kwamba mataifa ya nje wao ni werevu, lakini kama wangekuwa ni werevu na atlas wanazo kwanini kila wakati walipokuwa wanauliza Mlima Kilimajaro upo wapi wanasema huu upo nchi nyingine. Kwa hiyo, si kwamba lazima wawe werevu, walikuwa ni wajinga. Sasa Mheshimiwa Rais ametusaidia kuwaondolea ujinga waliokuwa nao wa kujua vivutio vipi vipo upande gani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tunataka kupata tija katika hilo our hospitality na tour guides wetu wanapaswa kuongezewa uwezo wapenzi. Bado hospitality yetu kama nchi haipo top watch. Kwa hiyo hili wizara husika na Serikali ikae pamoja ione kwamba tunahitaji ku-improve sana upande wa hospitality yetu pamoja na tour guides; hilo litatusaidia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, siku za karibuni tumeona wachezaji wakubwa wa vilabu vikubwa vya Ulaya wakija, na wanakuja Serengeti; lakini hawa pia tunawaona wakati wa mapumziko yao ya wakati wa kiangazi wakienda kupata mapumziko katika fukwe na hasa za Bahari ya Mediterranean Barbados pamoja na Dubai. Kwanini sisi, yaani tunajua wanalolitaka tuna joto lote na jua lote na mchanga wote wanaoutaka, kinapungua nini Tanzania? Hatujaweza kuimarisha beach sports, maana ndicho wanachokitafuta.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na pale Pwani ya Dar es Salaam kuna visiwa vizuri; kwanini Serikali isione kwamba kuna sababu ya ku-improve mazingira ya uwepo wa visiwa katika ufukwe wa Dar es Salaam halafu ikaingia pamoja na sekta binafsi ku-improve beach sports ili tuwateke waje Serengeti wakimaliza wapumzike pale kwenye beach zetu? Kwa hiyo kuna sababu ya kuanzisha kile wanachokitapata katika Bahari ya Mediterranean visiwa vya Ibiza, Barbados na Dubai tukilete pale Dar es Salaam ili waweze kukaa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine katika ku-improve habari ya utalii; watu wengi sana tunapokwenda katika miji unasema kwamba nita spend siku moja ya ziada au ya pili kwa ajili ya shopping au kwa ajili ya kuangalia mji, lakini miji yetu haijatoa hayo mazingira. Kwa hiyo, watalii wanakuja wanaishia Serengeti wanapanda ndege na kuondoka; na sababu kubwa ni kwasababu hatuna museums zinazovutia. Yaani tuna museum lakini yawezekana vilivyomo ndani ya museum haviwavutii kusema kwamba nita spend siku moja Arusha, nita spend siku moja Dar es Salaam kwa ajili ya kuangalia, what’s is there to see hatujaweza kuwapa hicho watalii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nilikuwa napendekeza kwamba, mbona Tanzania tunavyo vitu vya kuwapa? Kwa mfano; tumekuwa tukiongea katika hili Bunge juu ya mjusi yule wa Tendaguru aliyoko Ujerumani. Kwani Tendaguru siniyakwetu? na Tendaguru ambayo hamuijui vizuri kijiolojia ni mahali ambapo katika Bara la Afrika ndipo panapoongoza kuwa na masalia ya wale mijusi na viumbe wale wa zamani. Kwa hiyo, haya mabaki yalichimbwa mwaka 1905. Hivi Serikali ilishawahi kuwekeza kiasi kwamba tuone kama tunaweza tukachimba na sasa tukapata mjusi wetu wa kuchimba sisi wenyewe? Maana yule alichimbwa na Wajerumani karne imepita sasa. Kwa hiyo, mimi ninapendekeza Serikali iweke fedha katika utafiti pale Tendaguru ili ikiwezekana watu wetu wa archeology waende pale wajaribu kuchimba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naelewa kwamba kazi ya kumuunganisha ni kazi kubwa sana lakini tupate na sisi mifupa baadhi baadhi tuiweke katika museum yetu. Lakini pia jambo ambalo tunalo la kuvutia zaidi … (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)