Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023

Hon. Dr. Dorothy Onesphoro Gwajima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023

WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua muda huu kuwashukuru sana Wajumbe wa Kamati yangu ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii wakiongozwa na Mwenyekiti, Mheshimiwa Fatma Toufiq, Mbunge pamoja na Makamu wake Mheshimiwa Lulida pamoja na Wajumbe wote wa Kamati hii kwa uongozi wao, kwa maoni na mchango wao ambao umetuwezesha kufanikisha yale ambayo yamesomwa na Mwenyekiti hapa; kwamba kuna mafanikio yametokea kwenye Wizara hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa maono yake ya kuunda hii Wizara ambayo sasa naona inafariji sana kuona imemilikiwa na Waheshimiwa Wabunge na jamii, kwamba ilikuwa inahitajika na ndiyo maana hoja zinazidi kuongezeka na michango inaongezeka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba nijielekeze kwenye kutoa mchango wangu kwenye maeneo machache kutokana na muda. Kwanza ni suala la maendeleo na ustawi wa machinga ambalo limezungumzwa sana hapa na ikatakiwa tutoe maendeleo yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia kwamba Serikali inachukulia kwa uzito sana ajenda ya maendeleo na ustawi wa machinga ambapo sasa suala la database yao ambayo awali ilikuwa haikidhi mahitaji limefanyiwa kazi na tunakuja na mfumo wa kidijitali ambao umeshakamilika kwa ajili ya kutoa vitambulisho. Vitambulisho hivyo vitasomana na mifumo mingine ikiwepo Kitambulisho cha Taifa, anwani za makazi, taasisi za fedha, bima za afya na mifuko ya hifadhi ya jamii. Kwa hiyo ni kitambulisho bora kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninavyosema hapa wiki ijayo tunazindua mafunzo hayo ili wataalamu sasa warudi kwenye jamii kwenda kuwaelimisha wamachinga waanze kujisajili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo, fedha zile ambazo ni za mikopo zimesemwa sana hapa, kwa ajili ya wamachinga, benki zimeshatoa majibu; na sasa hivi Kamati inafanya uchambuzi kwa kushirikiana na Wizara ya Fedha ili ile benki ambayo imeonyesha unafuu kulingana na mahitaji yetu ianze kutoa ile mikopo. Kwa hiyo kuna mambo yanaendelea hapa. Mpango wetu ni ifikapo mwezi wa tatu hivi vitambulisho wawe tayari wameshaanza kupewa na hiyo mikopo waanze kuipata.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba pia kusema kuhusu WDF; WDF ni mfuko wa wanawake wa maendeleo ambao Wizara ulikuwa unaitoa. Ulianza tangu mwaka 2015/2016 lakini mtaji wake ulikuwa shilingi bilioni 1.3. changamoto zilezile zilizokumba mfuko wa 4.4.2 ule wa Halmashauri, kuanzia kwenye vyanzo vyake, uliukumba na huu mfuko watu wakawa wanakopeshwa hawarejeshi. Tuna madeni yanayokaribia shilingi milioni 500 ambayo yako kwenye Halmashauri, haya tunayafuatilia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunajirudisha kujiunganisha na huu mfumo wa kidijitali wa wamachinga ili kuanza sasa kuwasajili na wanawake ambao wataanza kuzipata zile fedha ambazo zingine ziko benki kama shilingi milioni 254 na zingine zipo kwenye mkopo unaozunguka. Kwa hiyo, tutaurejesha huu na tutausemea sana ili wanawake hawa waweze kupewa hii mikopo kupitia utaratibu wa vitambulisho hivi vilivyoboreshwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kumalizia maneno machache kuhusu NGOs hizi ambazo zinazoonekana hazizingatii sheria, miongozo na taratibu za nchi yetu. Hizi tunazifuatilia kupitia kuimarisha majukwaa ya Halmashauri yatakayoongozwa na Waheshimiwa Wakuu wa Wilaya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, huyu Mtaalamu wa Maendeleo ya Jamii anayeongoza Dawati la NGO, watafufua majukwaa haya. Kwa hiyo itakuwa Halmashauri palepale inaimarisha ufwatiliaji na wale wanaoenda kinyume wanatolewa taarifa na huyo Msajili Msaidizi aliyeko kwenye Halmashauri anachukua hatua na siyo kusubiri mpaka jambo liwe kubwa katika ngazi ya kitaifa. Tunaimarisha hizi regulatory mechanisms katika Halmashauri zote nchini, tumeshaongea na TAMISEMI na barua zilishakwenda, sasa ni ufUatiliaji. Mengine tutawasilisha kwa maandishi, nashukuru.