Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023

Hon. Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kupata nafasi hii. Kwa sehemu kubwa sana nitachangia kwenye Kamati ya Utawala, Katiba na Sheria.

Kwanza, napenda kuunga mkono hoja lakini nipongeze Kamati zote mbili ambazo zimetoa wasilisho lake leo, na maalumu kwa Kamati ya Utawala, Katiba na Sheria, kwa hoja mbalimbali ambazo zimetolewa mapendekezo na maazimio.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Katiba na Sheria inaungana kwa ujumla wake juu ya mapendekezo yote yaliyotolewa na Kamati hii ya Utawala Katiba na Sheria na hasa kwenye maeneo yafuatayo; moja, majengo ya Mahakama ya Mwanzo yaboreshwe kwa kufanyiwa ukarabati. Tunapokea ushauri. Vilevile, tunataka tu kulijulisha Bunge lako Tukufu kwamba, majengo mengi ya Mahakama za Mwanzo ni ya miaka mingi sana. Mengi yamejengwa kati ya miaka ya 1950 – 1960. Mengine yamerithiwa. Mahakama hizi zote, hasa zile za majengo yasiyokarabatika, haya tunakwenda kubadili na kuyajenga majengo mapya na kasi ya ujenzi ni kubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili lililotolewa kama ushauri kwa Serikali, Serikali ijenge majengo ya Mahakama za Mwanzo kwenye maeneo ambayo hayana Mahakama za Mwanzo. Zoezi linaendelea. Tayari Mahakama za Mwanzo zipatazo karibia 60 zilishafanyiwa kazi, na kwa kipindi hiki cha fedha 2024/2025, zinakwenda kujengwa Mahakama za Mwanzo 32 katika maeneo mbalimbli hapa nchini. Nawaomba Waheshimiwa Wabunge ambao maeneo yao hayajafikiwa na majengo mapya, majengo yanakuja. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu katika eneo hili ni matumizi ya TEHAMA. Napenda tu kuwaeleza Waheshimiwa Wabunge, Mahakama yetu ya Tanzania imefanya mageuzi makubwa sana kwenye eneo la TEHAMA. Mtakubaliana nami, kwamba katika maeneo yote ya Mahakama ambazo zinaanzia ngazi ya wilaya kupanda juu mpaka kwenye Mahakama Jumuishi, Kamati ya Utawala, Katiba na Sheria imepita kwenye majengo ambayo sasa yako kwenye TEHAMA ya kisasa kabisa. Tuwaahidi tu kwamba, kwenye Mahakama hizi za Mwanzo kadiri zinavyoendelea kufanyiwa marekebisho makubwa ya ujenzi, TEHAMA inaenda kuchukua nafasi yake kwa sababu, karibu Mahakama zote nchini hilo ndilo lengo lake la msingi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikija kwenye eneo lingine ambalo Kamati imetoa maazimia yake, ni eneo ambalo imeshauri kutumia wale wanasheria wa halmashauri hapa nchini. Ushauri wao umepokelewa ingawa utapitiwa upya kwa sababu, yule mwanasheria wa halmashauri ni mwawakilishi wa AG kama ilivyo kwa sisi hapa Bungeni. Kwa hiyo, tunakwenda kupitia yale maeneo ambayo kimsingi yasije yakaleta usumbufu kwa wananchi kwa sababu hawa wanatakiwa kuwa neutral wakati watu wawili wanapogombana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na tunashukuru sana na tunaunga mkono hoja. (Makofi