Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023

Hon. Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023

NAIBU WAZIRI WA FEDHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana na awali ya yote nami niungane na wenzangu katika jambo la kumshukuru Mwenyezi Mungu Rahim, Mwenyezi Mungu ambaye ametujaalia rasilimali ya uhai hadi sasa tunaendelea nayo, kwani ndiyo thamani peke yake ya binadamu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili napenda kumshukuru sana na kumpongeza Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kazi kubwa ambayo naifanya katika nchi yetu hii. Nawapongeza sana Wenyeviti ambao wamewasilisha leo taarifa zao. Kwa kweli wamewasilisha kwa ufanisi na weledi mkubwa sana. Nawapongeza sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, nawapongeza Wajumbe wa Kamati hizo pamoja na Wabunge wenzangu kwa namna wanavyochangia hoja katika kujenga Taifa hili. Ni Wabunge wengi ambao wamechangia katika hoja tofautitofauti ambazo ni hoja nzuri na za msingi kabisa. Miongoni mwa hoja hizo zimegusa kwa njia moja ama nyingine Wizara ya Fedha. So, niseme kwamba hoja zote ambazo zimetolewa, maoni na ushauri ambao umetolewa tumezipokea kama Serikali na tunaenda kuzifanyia kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa uchache kabisa kwa sababu ya muda, naomba nijielekeze tu moja kwa moja kwenye suala zima la miundombinu ya barabara ambayo imetajwa na Wabunge wengi katika Taasisi yetu ya TARURA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iliahidi kuongeza bajeti kwa kiasi cha shilingi bilioni 350 ili kutatua changamoto za miundombinu ya barabara katika halmashauri zetu zote nchini. Kwa sasa, Serikali kupitia TARURA ipo kwenye hatua za ununuzi ili miradi hiyo iweze kutekelezwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa miradi ya barabara inatekelezwa kwa kipindi cha miezi sita hadi miezi 18 (mwaka mmoja na nusu). Wizara ya Fedha kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais, TAMISEMI, itahakikisha fedha za malipo ya awali (advance payment) inalipwa kwa wakati unaostahiki mara tu baada ya mikataba hiyo kusainiwa. Hivyo, naomba nikuhakikishie na nilihakikishie Bunge lako Tukufu pamoja na Waheshimiwa Wabunge kwamba, fedha hiyo ya miradi hiyo ambayo imetajwa, kiasi cha shilingi bilioni 350 zitatekelezwa kama ilivyopangwa na ilivyoahidiwa na Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba nirudie kukuhakikishia kwamba, Wabunge waondoe shaka katika hili. Fedha hiyo itatolewa kwa wakati kabisa ili kutekeleza miradi hiyo. Ahsante sana. (Makofi)