Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023

Hon. Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia fursa ya mimi leo kuchangia. Kwanza kabisa nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kazi kubwa anayoendelea kuifanya, pia ninampongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Naibu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila kumsahau Mheshimiwa Dkt. Tulia Ackson, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kazi kubwa anayoendelea kuifanya na kutuwakilisha vema katika Bunge letu hili Tukufu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo ninataka nichangie mambo machache tu kwenye Wizara hii ya Serikali za Mitaa - TAMISEMI. Kwanza kabisa sisi Wanajimbo la Msalala tunazo shukrani nyingi kwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa fedha nyingi sana alizotupatia za maendeleo kwenye Jimbo la Msalala. Ametupatia fedha nyingi kwenye sekta ya afya, tunatakribani ya vituo vipya sita vya afya ametuletea, tuna zaidi ya zahanati 34 zimekamilika lakini juzi nimeenda kukabidhi ambulance mpya kwa niaba ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ambayo itaenda kuhudumia wananchi wagonjwa wa Kata ya Isaka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hajaishia hapo kwenye sekta ya elimu ametupa fedha nyingi sana, tuna shule zaidi ya saba mpya, hajaishia hapo ametuongeza fedha nyingine ya kujenga Chuo cha Veta bilioni mbili na chuo sasa hivi kinaenda vizuri sana. Hajaishia hapo ametupa fedha za kujenga Chuo cha Nursing na chenyewe kimekamilika, hivi karibuni tunaenda kupokea wanafunzi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ndani ya miaka minne, ndani ya miaka mitatu ya Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan tunaenda kuwa na vyuo viwili kwenye Jimbo la Msalala. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni ukweli usiopingika kwamba Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan anatafuta fedha nyingi sana kwa uchungu mkubwa, kwa wivu mkubwa kuhakikisha ya kwamba wananchi wa Jimbo la Msalala na nchi nzima wananufaika na miradi mbalimbali kwenye maeneo hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nianze kwa kuunga mkono maazimio haya ya Kamati na nimpongeze sana Mwenyekiti wa Kamati hii kwa maazimio mazuri kabisa, maazimio yenye afya ambayo ninaimani kabisa kama yataenda kutekelezeka basi kutakuwa na mabadiliko makubwa sana kwenye sekta hii ya TAMISEMI. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa mimi nakubaliana moja kwa moja na suala zima la mapendekezo ya Kamati ya kupitia upya Kanuni ya uendeshaji wa Mabaraza yetu ili kuona namna gani sasa Waheshimiwa Wabunge wanashiriki vema kwenye shughuli za maendeleo kwenye maeneo hayo. Ukweli usiopingika ni kweli Mheshimiwa Mbunge ni Diwani na ni Mjumbe wa Kamati ya Fedha lakini kiuhalisia huu uhalisia wa Mheshimiwa Mbunge kuwa Mjumbe wa Kamati ya Fedha na kuwa Mjumbe wa Baraza mara nyingi kalenda ya upangaji wa vikao kwenye maeneo hayo hatushirikishwi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe sana Waziri yuko hapo ni namna gani sasa mje na mkakati wa kutoa maelekezo au mwongozo wa kupeleka kule kwenye Halmashauri upangaji wa vikao hivi vya Kamati ya Fedha na Mabaraza uzingatie ratiba ya Waheshimiwa Wabunge kuwepo kule ili tuweze kushiriki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge anakuwa anakuwa vizia Kikao cha Kamati ya Fedha, anavizia Baraza, ukikaa Jimboni muda wote uko Jimboni, lakini ratiba ya Bunge ikitoka tu ukiwa safarini kuelekea Dodoma unapokea message kwamba kesho kuna Kamati ya Fedha, kesho kuna Baraza, hivi wanaogopa nini kutoa ratiba wakati Mheshimiwa Mbunge akiwa yuko Jimboni ili aweze kushiriki kama Mjumbe halali wa Kamati ya Fedha, aweze kushiriki kama Mjumbe wa Baraza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapeleka fedha nyingi sana kule chini na wengi mmeona, ninampongeza Katibu wetu Mwenezi amefanya ziara kwenye maeneo hayo, amekuta changamoto nyingi sana na ninataka niseme na Mheshimiwa Naibu Waziri Mkuu yuko hapo. Mheshimiwa Rais anapeleka fedha nyingi sana kwenye Majimbo yetu lakini wasimamizi walioko kwenye maeneo haya na hasa aliowapatia dhamana, hawatimizi majukumu yao ya kusimamia kazi vizuri, wanamuhujumu kwenye maeneo ya miradi huko chini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, fedha zinazokwenda huko nitolee mfano kwenye Jimbo langu mimi, tumepokea fedha nyingi sana. Juzi tumebaini wizi wa fedha kiasi cha shilingi milioni mia mbili na wezi wamekatwa wamekula Fedha za TASAF, wazee ambao hawawezi kufanya shughuli. Mheshimiwa Rais ametafuta fedha amewapelekea hawa akinamama wanyonge kwa ajili ya TASAF lakini baadhi ya watumishi wachache ambao siyo waaminifu wameenda kula zile fedha na nini kimefanyika? Hakuna hatua yeyote iliyochukuliwa isipokuwa ni kwamba kaeni hapa, kila mwisho wa mwezi tutawakata kwenye mshahara wenu laki moja moja. Hivi fedha hizi anazozitafuta Mheshimiwa Rais kwa uchungu, anapeleka huko ili zikawahudumie wananchi, watu baki wanakula fedha na hakuna hatua madhubuti zinazochukuliwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe sana Mheshimiwa Naibu Waziri Mkuu niiombe Serikali ikiwezekana iweze kutoa mwongozo kwa sasa na hasa kwa kipindi hili tulichopo. Mheshimiwa Rais amewaamini watu kule wasimamie shughuli za maendeleo kule chini, lakini watu hao ni ukweli usiyopingika kwa wakati huu wanatumia gari za Serikali ambazo zingetumika kwenda kutatua migogoro, wanatumia mafuta ya Serikali ambayo yangetumika kwenda kutatua migogoro, wanaanza kwenda kutafuta kura na watu hawa Mheshimiwa Naibu Waziri Mkuu utoke mwongozo wa kuwaambia kama kuna watu ambao wanahitaji kumsaidia kumsaidia Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa sasa wajitokeze kumsaidia kwa ukweli na wale ambao wanawaza kwenda kugombea Majimbo waache kazi zile waende wakagombee Majimbo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wanatumia fedha za Serikali, wanatumia magari ya Serikali, wanaenda kuanza kukimbizana na Wajumbe kwenye maeneo hayo, niombe sana Mheshimiwa Naibu Waziri Mkuu, hebu Serikali sasa itoe mwongozo wale watakao taka kumsaidia Dkt. Samia Suluhu Hassan ili miradi iweze kukamilika huko chini. Tunaenda kwenye uchaguzi, miradi mingi haikamiliki na wale wazembe ambao wanakula fedha hatua kali zichukuliwe ili kuhakikisha ya kwamba miradi ile inakamilika. Mheshimiwa Naibu Waziri Mkuu niombe sana hili liweze kuchukuliwa hatua kali ili tuweze kumsaidia Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye maeneo hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nizungumzie suala zima la vituo vya afya; siku zote mimi huwa nasema katika uanzishwaji wa vituo vya afya hivi huduma inayotolewa kwenye vituo vya afya mara nyingi hakuna huduma inayotolewa bure ni huduma ya malipo. Huwa najiuliza na mara nyingi huwa nakaa nao kuona kwamba kuna utofauti gani kati ya vituo vya afya (dispensary za private) na vituo vya afya vya Serikali, huduma ni zilezile. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaiomba Serikali njooni na mkakati wapeni Ma-DMO na in-charge wa kwenye vituo vya afya hivyo kipimo kwamba kipimo cha in-charge kwenye Kituo cha Afya A ni kuhakikisha ya kwamba anakusanya mapato, anasimamia mapato vizuri, pia ahakikishe kwamba dawa zinapatikana wakati wote hiyo inawezekana na ikiwezekana kwa sababu mmeshagatua madaraka yako huko maana yake kwenye mapato lindwa wanaruhusiwa kukusanya mapato na kutumia, waweze basi kuajiri, kwenye vituo vya afya hivyo…

MWENYEKITI: Mheshimiwa ahsante sana, malizia mchango wako, muda wako umeisha.

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. (Makofi)