Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge kuhusu Wakala wa Kimataifa wa Kimataifa wa Nishati Jadidifu (International Renewable Energy Agency - IRENA) na Azimio la Bunge kuhusu mapendekezo ya kuridhia Mkataba wa Kuanzisha Taasisi ya Dawa ya Afrika wa Mwaka 2019 (Treaty for the Establishment of the African Medicine Agency - AMA)

Hon. Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Bunge kuhusu Wakala wa Kimataifa wa Kimataifa wa Nishati Jadidifu (International Renewable Energy Agency - IRENA) na Azimio la Bunge kuhusu mapendekezo ya kuridhia Mkataba wa Kuanzisha Taasisi ya Dawa ya Afrika wa Mwaka 2019 (Treaty for the Establishment of the African Medicine Agency - AMA)

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi kutoa mchango wangu katika mkataba huu wa kuanzishwa kwa Taasisi ya Dawa ya Afrika ya mwaka 2019. Ni ukweli usiopingika kwamba sisi kama nchi tumechelewa. Kati ya nchi hamsini na tano zilizokaa mwaka 2019 kupitisha azimio hili la kuwa na Taasisi hii sisi tumechelewa sana. Leo ndiyo Serikali yetu imeleta Bungeni ili tuweze kujadili na kuridhia mkataba huu.

Mheshimiwa Naibu Spika, binafsi naomba niunge mkono hoja, na niwashauri na kuwaomba Waheshimiwa Wabunge wenzangu kwamba turidhie mkataba huu kwa sababu una manufaa kwa Taifa letu la Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaona kwamba Rwanda imepata nafasi au fursa ya kuweza kujenga Makao Makuu ya Taasisi hii. Labda na sisi Tanzania tungeridhia miaka sita iliyopita tangu mkataba huu wamekaa mezani na kusaini na kuridhia kwamba waanzishe Taasisi hii inawezekana kabisa sisi nchi yetu ingekuwa miongoni mwa nchi ambayo kungekuwa na hii Taasisi. Kwa sababu tuna Mamlaka ya Dawa na Tiba ambayo ni bora sana katika Bara la Afrika kwa sababu inakidhi iko katika kiwango cha tatu cha umahiri, na WHO imepitisha.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo mimi sitakuwa na mambo mengi ya kuzungumza katika mkataba huu; ni mkataba ambao unatija ni mkataba ambao utahimarisha na utadhibiti na kufuatilia masuala yote ya umahiri ya ufanisi wa dawa zote ambazo zitakuwa zinatumika katika bara letu la Afrika hususani Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwa na dawa nyingi ambazo zinatengenezwa. Nyingine zinatengenezwa na sisi Watanzania kienyeji na zinaingia Tanzania, zinatumika kwa wananchi wetu. Lakini tukishakuwa na taasisi ambayo inadhibiti na kusimamia popote zitakapotoka na popote zitakapokwenda zitakuwa zimehakikiwa, kudhibitiwa, kuwa na ubora halisi na hazitaleta madhara kwa wananchi wetu. Hata kama kutakuwa na madhara basi taasisi hii itakuwa na uwezo wa kudhibiti yale madhara ambayo yatatokana na hizo dawa ambazo wananchi watakuwa wanazitumia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo basi niombe kwa mara nyingine, kwa mikataba mingine ambayo ina manufaa kwa Taifa letu. Serikali ijitahidi kuwezesha, kusukuma hili suala ili mikataba kama hii ambayo inajenga na yenye manufaa kwa Watanzania na kwa nchi, inapokuwa imetolewa wailete mapema, waishughulikie, waichakate na ije kwa wakati. Miaka sita toka 2019 mpaka leo ndipo Mkataba unaingia Bungeni binafsi naona kwamba tumechelewa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimshukuru Mheshimiwa Rais ambaye ndiye Amir Jeshi Mkuu anaendesha nchi hii kwa sasa hivi. Tangu mwaka 2021 mpaka leo ni kama mwaka mmoja au miaka miwili mkataba umeweza kufika Bungeni; lakini tangu 2019 mkataba uko kwenye mchakato hatujaridhia. Hivyo basi niwashawishi Wabunge wenzangu kwamba mkataba huu kuundwa wa taasisi hii tuweze kuridhia ili na sisi tuwe miongoni mwa nchi hamsini na tano za Afrika ambazo tumeridhia na tutanufaika na mkataba huu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo ninaunga mkono hoja, ninakushukuru sana. (Makofi)