Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge kuhusu Wakala wa Kimataifa wa Kimataifa wa Nishati Jadidifu (International Renewable Energy Agency - IRENA) na Azimio la Bunge kuhusu mapendekezo ya kuridhia Mkataba wa Kuanzisha Taasisi ya Dawa ya Afrika wa Mwaka 2019 (Treaty for the Establishment of the African Medicine Agency - AMA)

Hon. Dr. Josephat Mathias Gwajima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kawe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Bunge kuhusu Wakala wa Kimataifa wa Kimataifa wa Nishati Jadidifu (International Renewable Energy Agency - IRENA) na Azimio la Bunge kuhusu mapendekezo ya kuridhia Mkataba wa Kuanzisha Taasisi ya Dawa ya Afrika wa Mwaka 2019 (Treaty for the Establishment of the African Medicine Agency - AMA)

MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, na mimi naomba nikushukuru sana kwa kunipa nafasi kuchangia katika hoja hii. Kwa makusudi ya kuokoa wakati nitaenda moja kwa moja kwenye Azimio la Bunge kuhusu kuanzisha kwa Taasisi ya Dawa ya Afrika.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa maana kwamba tarehe 11 Februari, 2019 ni mahala ambapo Umoja wa Nchi za Kiafrika na wakuu wa nchi walikubaliana kwa pamoja kuanzishwa kwa Taasisi hii ya Dawa ya Afrika. Kwa hiyo nimshukuru sana Mheshimiwa Rais Mama Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwa sehemu ya viongozi hawa na kukubaliana kwenye Mkataba huu wa muhumu sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, dawa ni matibabu katika ulimwengu wa leo lakini pia dawa ni silaha katika ulimwengu wa leo. Tunapozungumza kuhusu dawa inatoka mahala ambapo si nchini kwetu na inakuja nchini kwetu kwa lengo la kutibu watu ni maeneo muhimu sana kwenye component ya nchi ili tuwalinde watu wetu wawe salama leo, kesho na siku zijazo. Na kwa sababu hiyo nimeona moja ya sababu ya manufaa yanayotokana kuridhia kwa mkataba huu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, manufaa ya kwanza ni kuhimarika kwa mfumo wa udhibiti na kuweza kudhibiti bidhaa ambazo haziwezi kudhibitiwa kwa naamna ya kawaida. Wametoa mfano kama bidhaa zinazotokana na genetic au genetic connections. Ninaomba nitoe mfano kwa jambo ambalo nalifahamu vizuri sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hivi kuna aina ya matibabu yanaitwa genome editing by Crispr technology. Genome editing by crispr technology ni aina ya matibabu ambayo unamtibu mtu mwenye selimundu (sickle cell) kwa kutumia utalamu wa ku-edit gene yake. Ndugu yangu Daktari Mollel anafaahamu vizuri sana. Matibabu haya ni kwamba una-edit gene ya mtu na unaondoa ule uwepo wa selimundu kwenye genetic inheritance yake ili umtibu. Haya ni matibabu yanayotokana na genetic lakini pia ni matibabu yanaweza kuwa na madhara makubwa kwa nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano kwenye genetic editing by crispr technology ni kwamba utu wa mtu upo kwenye gene ya mtu. Ukifanikiwa ku-edit gene ya mtu unaweza ku-edit utu wa mtu, unaweza ku-edit urefu wake, saizi ya kichwa chake, uwezo wake wa kuelewa, IQ yake, intellectualism yake, rangi ya ngozi na utu wake kwa ujumla.

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi Waafrika haatuna maabara za kutosha za kuweza kuchuja kila kitu kinachotoka kwa wenzetu kule magharibi. Sasa kwa Mataifa ya Kiafrika kuja pamoja na kuwa na azimio ya kuanzisha Umoja wa Dawa za Kiafrika inasaidia sana mataifa ya Kiafrika kuwa na maabara ya pamoja kwa ajili ya kudhibiti mambo yenye lengo ya kuiangamiza Afrika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo hata kabla sijaenda mbali ninaunga mkono azimio kwa asilimia mia moja pamoja na hayo machache nitakayoyaelezea. Ninaomba ni-highlight jambo moja; katika kila dawa inayotoka nje ya Afrika inaingia kwenye nchi kila nchi inakuwa na jukumu ya ku-analyze hiyo dawa, kujua usalama wake, kujua madhara yake kwa siku za karibuni, siku za kati na siku za mbele. Lakini kama unavyojua kwa mapato ya nchi ya Kiafrika ni nchi za Kiafrika chache sana zenye uwezo wa kufanya jambo hilo.

Mheshimiwa Naibu Spika, unakumbuka tulipokaribiwa na chanjo ya COVID-19 tulivyoanza kurukaruka hapa; hakuna Mzungu aliyekuwa tayari kutupa intellectual property ya hiyo chanzo. Lakini tungekuwa tumeishatengeneza tayari Jumuiya ya Kiafrika ya kuziangalia hizi dawa kwa pamoja tungekuwa na maabara za pamoja za Kiafrika zinazochuja dawa zetu zitumikeje na kwamba zina madhara gani kwa siku za karibuni, siku za kati, na siku za usoni. Kwa hiyo azimio hili lazima tuliliridhie kwa haraka na kwa usahihi kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema dawa inatibu lakini pia dawa ni silaha. Nimshukuru sana Mheshimiwa Rais wa Jumuhuri ya Muungano ya Tanzania kwa maana hii yeye na wakuu wa nchi wenzake tarehe 11 Februari, 2019 walipoamua kusaini mkataba huu na sisi sasa kama Bunge tunatakiwa kuazimia na kuridhia. Mimi ninalishawishi Bunge lako tuazimie kwa haraka, tuwe na Jumuiya hii ya pamoja, tuwe na maabara za pamoja ili dawa zote zinazotoka nje ya nchi ya Afrika tuwe na uwezo wa kuzichuja na kujua zinawasaidiaje watu wetu; na kama zina madhara iwe ni rahisi kuwa na jukumu la pamoja kama Waafrika kudhibiti na kwenda kwa pamoja.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Naomba azimio hili lipite, ahsante sana. (Makofi)